Ijumaa, 5 Agosti 2016

*JINSI YA KUTUMIA MUDA VIZURI KWA AJILI YA MAFANIKIO YAKO YA KESHO*

Hivi Ndivyo Unavyoweza Kutumia Muda Wako Vizuri Na Kukuletea Mafanikio Makubwa.
Muda ni ma li! Huu ni usemi maarufu sana kwa vijana na wazee. Unaonekana ni usemi wa kawaida na uliozoeleka kwa watu wengi, maskini na matajiri, wanawake na wanaume. Japokuwa watu wengi tunautumia usemi huu, lakini baadhi yetu hatuelewi maana yake na wengi wetu hatuutumii katika maisha yetu.
Muda ni mali maana yake kila kitu, vitu vyote vinavyoonekana vidogo na vikubwa ni matokeo ya matumizi ya muda. Hata mimi na wewe ni matokeo ya matumizi mazuri ya muda. Kila mafanikio yaliyowahi kutokea na yanayoendelea kutokea ni matokeo ya matumizi mazuri ya muda. Kwa hiyo kuna uhusiano mkubwa sana kati ya mafanikio na matumizi ya muda,yaani muda ukitumika vizuri mafanikio yanapatikana na muda huo huo usipotumika vizuri hakuna mafanikio.
Hakuna haja ya kueleza na kufafanua maana ya muda, ila nataka ujue kuwa kuna aina za muda, ndiyo zipo aina mbili za muda. Aina ya kwanza ya muda ni MUDA WA SAA. Muda huu unaanzia sekunde hadi mwaka. Katika muda wa saa, tunaposema miaka miwili ni miaka miwili, haizidi wala haipungui.Tunaposema huyu ana miaka hamsini ina maana mtu ameishi vipindi hamsini ambapo kila kipindi kina jumla ya miezi kumi na mbili, haizidi wala haipungui.
Aina ya aili ya muda ni MUDA HALISI. Muda halisi unaundwa na muda wa saa na matukio. Katika aina hii ya muda tunaangalia matukio yaliyotokea katika muda wa saa husika.Tunalinganisha idadi ya miaka na miezi na matukio au mafanikio yaliyopatikana katika kipindi husika. Watu wanaweza kuwa sawa katika muda wa saa lakini wakawa tofauti katika muda halisi. Mtu anaweza kuwa na umri wa miaka sitini(katika muda wa saa) lakini akawa kwa mafanikio ni kama mtu aliyeishi miaka thelathini tu.
Na pia mtu mwingine anaweza kuwa na umri wa miaka thelathini, lakini akawa na mafanikio makubwa sana kimaisha kama mtu aliyeishi miaka mingi sana duniani, yawezekana hata miaka sabini. Usichanganyikiwe, nalinganisha muda wa saa na mafanikio. Muda halisi unatuambia kwamba kuna kuchelewa katika maisha. Muda halisi unatukumbusha kuwa kuna wakati tunaweza kupoteza miaka yetu bila kujua. Unatukumbusha kufanya jambo sahihi kwa wakati sahihi.
Tumejifunza aina za muda na tofauti zake, sasa tuangalie matumizi ya muda wa saa.Tunatumia muda huu kufanya mambo matatu ambayo yanatuleta kwenye muda halisi, tukiwa tumewahi au tumechelewa tunatumia muda katika
kufikiri, kusema au kuzungumza na kufanya mambo mbalimbali katika maisha yetu.
Baada ya kuangalia matumizi ya muda wa saa, tumegundua kuwa tunautumia muda kama chombo kutusafirisha kutoka katika ulimwengu wa namba na mahesabu kwenda kwenye ulimwengu wa halisi,ulimwengu wa vitendo ambapo tunaweza kufanya tathmini na kuona kuwa tumewahi au tumechelewa, tuko nyuma au tuko mahali sahihi.
Sasa tuangalie mambo ya kufanya ili tuweze kuutumia muda wa saa na kufikia mafanikio ambayo yataweka uwiano sawa kati ya muda wa saa na muda halisi katika maisha yetu.Yapo mambo mengi ambayo unapaswa kuyafanya ili uweze kutumia muda wako vizuri, baadhi ya  mambo hayo ni haya yafuatayo:-
1. Weka kumbukumbu ya mambo unayofikiria, unayoyasema na kutenda.
Kumbukumbu ni muhimu sana katika maisha ya binadamu kwa sababu ndizo zinazotusaidia kufanya tathmini. Jitahidi kuweka kumbukumbu za mambo unayofikiri, unayosema na kutenda japo kwa siku moja. Mwisho wa siku jitahidi kukukumbuka mambo uliyofikiria, uliyosema na kutenda yawe mazuri au Mabaya. Hii itakusaidia kufanya tathmini ya matumizi ya muda kwa siku hiyo.
Tathmini hiyo itakusaidia pia kujua umetumia muda vizuri au vibaya. Mara nyingi sana siyo rahisi kukukumbuka mambo yote uliyofikiria na kusema lakini ni rahisi kukukumbuka matukio na mara nyingi matukio hutokana na kufikiri na kusema,kwa hiyo kukumbuka matukio ni njia rahisi zaidi yakukuwezesha kufanya tathmini ya siku nzima.
2. Weka ratiba ya siku nzima.
Ratiba ni muhimu sana katika maisha ya kila siku.Usianze siku bila kujua utafanya nini siku hiyo. Unaweza kuweka na kupanga ratiba ya siku inayofuata kabla ya kulala au asubuhi kabla hujaanza jambo lolote. Watu wote waliofanikiwa, wamefanikiwa kwa sababu ya matumizi mazuri ya muda, wanafanya kazi zao kwa ratiba na wana nidhamu linapokuja swala la matumizi ya muda. Bila kuwa na ratiba muda hutumika bila mpangilio na wakati mwingine muda hupotea bure. Unapoweka ratiba hakikisha kila kitu ulichokiweka kina wakati na muda wake. Kinaanza saa ngapi na kuisha saa ngapi. Ni vyema ratiba hii iwe na mambo ya msingi tu. Usisahau mapumziko. Mapumziko ni muhimu kwa utendajibora wa akili na mwili.
3. Epuka kuwa na mipango mingi.
Katika ratiba yako usiweke mambo mengi sana ambayo utekelezaji wake ni mgumu au yanachosha.Weka mambo machache ambayo yanakupa nafasi ya kupumzika na kutafakari namna ya kuianza siku inayofuata. Ukiweka mambo mengi kuna hatari ya kuyatekeleza nusunusu na mengine yanaweza yasitekelezwe kabisa.
4. Usiruhusu mambo yasiyo ya msingi kuingilia ratiba yako.
Mara unapoanza kutekeleza mipango ambayo iko kwenye ratiba yako, usiruhusu mambo yasiyo ya msingi kuingilia na kuvuruga ratiba yako. Kuwa na nidhamu na heshimu ratiba yako. Zipo dharura lakini si dharura zote zinahitaji kushughulikiwa papo .Kama dharura ni ya msingi na inahitaji kushughulikiwa papo hapo hamna tatizo.Jifunze kutambua na kutofautisha dharura zinazohitaji kushughulikiwa papo hapo na zile zinazoweza kushughulikiwa baada ya ratiba kukamilika.
Kuna watu ambao wako tayari kuvuruga ratiba zao na kuacha shughuli zao kwa sababu ya mambo yasiyo ya msingi kwa mfano kuangalia mechi na burudani zingine ambazo haziwasaidii katika maisha yao. Narudia tena,uwe na nidhamu heshimu ratiba yako.
5. Epuka kutumia muda mwingi kufanya mambo yasiyo ya lazima na yasiyo na faida.
Epuka kutumia muda mrefu kufanya mambo yasiyo ya msingi na yasiyo na faida kwa mfano kuchati kwenye mitandao ya kijamii, kuangalia mechi na burudani zingine wakati ambapo unatakiwa kufanya mambo ya msingi kwa ajili yako na jamii inayokuzunguka. Sina maana mitandao ya kijamii mibaya ila nasisitiza kuwa na kiasi na kuipa nafasi ndogo katika maisha ya kila siku. Kama utakuwa unawasiliana kwenye mtandao wa kijamii basi iwe kwa faida na si kupoteza muda .
Ninasema hivi kwa sababu hili limekuwa tatizo Kubwa sana kwa kizazi cha sasa hasa vijana, tena wanafunzi ambao wanatakiwa wasome kwa bidii wasipoteze muda hata kidogo. Muda wa kufanya mambo ya msingi utumike kufanya mambo ya msingi na mambo mengine yapewe nafasi ya pili au ya mwisho.
5. Tumia sehemu Kubwa ya muda wako kufanya mambo ya msingi.
Unashauriwa kutumia 75% hadi 80% ya muda wako kufanya mambo yenye tija kwako na kwa wanaokutegemea.Tumia sehemu Kubwa ya muda wako kufanya mambo yatakayokujenga na kukuimarisha kiakili,kijamii na kiuchumi. Fanya kazi za kukuingizia kipato, soma vitabu, magazeti, na majarida yatakayokuongezea maarifa na kupanua ufahamu wako.Ukiingia kwenye Internet soma vitu vinavyokujenga na siyo kufuatilia habari za watu maarufu huku hakuna cha maana unachopata.
Wengine wanaingia kwenye Internet kuangalia ili kuangalia picha za ngono na utupu. Watanzania wengi watu wazima ukiwauliza walisoma vitabu lini, hawakumbuki, wengine wanakwambia shule ya msingi na wengine sekondari, inasikitisha. Wengine hata wanaponunua simu, hawasomi vile vitabu vinavyoelekeza namna ya kutumia hiyo simu. Watu walio wengi sana kama ni kusoma wanapenda kusoma vitu ambavyo haviwasaidii sana katika maisha yao kama magazeti ya udaku.

Naomba niishie hapo kwa maelezo zaidi tuwasiliane #0673214813…………whatsApp

Alhamisi, 4 Agosti 2016

AFYA NA UREMBO

AFYA NA UREMBO.

muonekano wako unaongezwa haiba na tabasamu la midomo yako,Midomo mikavu haivutii si kwa wanaume au wanawake ni wakati wako kutumia bidhaa ALOE LIPS
Imetengenezwa kwa
~Aloe vera
~Asali
~Jojoba oil

Kwa faida zifuatazo.

~Kulainisha midomo mikavu na inayo chanika

~Kuondoa utando mweupe mdomoni

~Kuondoa weusi unaotanda midomoni

~Unaweza kuipaka kama mafuta usoni

~Unaweza kuipaka kwenye vidole kuondoa mpauko unaosababishwa na kutumia sabuni kali

~unaweza kuipaka unapo ng'atwa na wadudu (kuzuia uvimbe na miwasho )

~Unaweza kuipaka unapotokewa na harara.

Ni ALOE LIPS,yenye matumizi zaidi ya moja kwa kurudia urembo wako.

Kwa mahitaji yako tuwasiliane utaletewa popote ulipo.

………0673214813………WhatsApp

Jumatano, 3 Agosti 2016

SIRI ZA MAWASILIANO YANAYOFIKISHA UJUMBE

[19/06/2016 01:22] Violeth: Siri Za Kukuwezesha Kushawishi Mtu Yeyote Akubaliane Na Wewe....                                      
Mawasiliano ni moja ya misingi muhimu sana kwenye maisha yetu ya kila siku. Na pia ni moja ya mahitaji muhimu kama tunataka kuweza kufikia mafanikio makubwa kwenye jambo lolote ambalo tunalifanya. Kumbuka ya kwamba chochote unachotaka kinatoka kwa watu wengine, hivyo jinsi unavyoweza kuwashawishi na wakakubaliana na wewe ndivyo itakuwezesha kupata unachotaka. Na ushawishi unaanzia kwenye mbinu bora za mawasiliano ambazo mtu anakuwa nazo.
Watu wengi wamekuwa wakiwasukuma wengine ili kupata kile wanachokitaka. Na wamekuwa wakifanya hivi kwa kubishana, kutisha, kudanganya na hata kulaghai ili wapate wanachotaka. Kwa njia hizi inakuwa vigumu zaidi kwa watu kuwa tayari kutoa kile ambacho wengine wanakitaka. Ni kutokana na changamoto hii Daktari na Mwanasaikolojia Mark Goulston alipokuja na kitabu ambacho kina mbinu bora za ushawishi ambazo zinamwezesha mtu kupata kile anachokitaka kutoka kwa mtu yeyote. Daktari Mark anatumia taaluma yake na uzoefu wake kwenye kazi ya ushauri katika kutushirikisha mambo haya muhimu ya kuzingatia kwenye mawasiliano yetu.
Karibu tujifunze kwa pamoja;
1. Kila mtu ana mahitaji yake, matamanio yake na pia ajenda zake. Kila mtu ana siri yake ambayo anaificha, ambayo hataki wengine waijue. Na pia kila mtu yupo bize, ana msongo wa mawazo, na hana muda wa kumtosha kufanya kila anachotaka kufanya. Ili kuweza kwenda na hayo yote yanayoendelea kwenye maisha yake, mtu anajitengenezea ukuta ambao bila ya kujua hayo huwezi kumshawishi kwa jambo lolote. Kabla hujataka mtu afanye au akupe chochote unachotaka, anza kwanza kuvunja ukuta huu ambao kila mtu amejijengea.
2. Ushawishi unaenda kwa mzunguko ambao una hatua tano muhimu. Yaani kabla mtu hajashawishika kufanya chochote unachomwambia, anapitia hatua hizi tano ambazo unatakiwa kuzijua na kujua jinsi ya kumpitisha mtu kwenye kila hatua;
Hatua ya kwanza ni kumtoa mtu kwenye kukataa mpaka kuwa tayari kusikiliza. Wakati wowote mtu yupo kwenye hali ya kukataa, unahitaji kuwa na mbinu ya kumfanya akusikilize.
Hatua ya pili ni kumtoa kwenye kusikiliza mpaka kukufikiria. Hapa mtu anakuwa amesikiliza kile ulichomwambia, na kuna mbinu bora za kumwambia na akaanza kufikiria kwamba anaweza kufanya au anaweza kuwa tayari.
Hatua ya tatu ni kumtoa kwenye kufikiria mpaka kuwa tayari kufanya. Baada ya mtu kufikiria kwamba anaweza kufanya anashawishika zaidi na kuwa tayari kufanya.
Hatua ya nne ni kumtoa kwenye kuwa tayari kufanya mpaka kufanya. Hapa ndipo mtu anapofanya kile ambacho unataka afanye au anakupa kile ambacho ulitaka akupe.
Hatua ya tano ni kumtoa kwenye kufanya mpaka kufurahia kufanya na kuendelea kufanya. Kufanya siyo mwisho wa mzunguko huu, bali mtu anahitaji kufurahia kwamba amefanya na kuendelea kufanya kadiri inavyohitajika.
Huu ndio mzunguko wa ushawishi ambao unatakiwa kuujua na jinsi ya kuutumia kwa watu mbalimbali. Utajifunza hayo kwenye kitabu hiki.
3. Ili uweze kuwa na ushawishi kwa wengine unahitaji kuujua vizuri ubongo wa binadamu. Ubongo wa binadamu umegawanyika kwenye sehemu kuu tatu ambazo zinatofautiana kwa miaka ambayo zimekuwepo.
Sehemu ya kwanza ni ubongo wa chini ambao una tabia kama za mjusi. Hii ni ile sehemu ya ubongo ambayo kazi yake kubwa ni kuhakikisha unaishi (kwa kiingereza survival). Ubongo huu kazi yake ni kuhakikisha umepata chakula na unaweza kujikinga na hatari. Ubongo huu huwa unachukua hatua haraka bila hata ya kufikiri kwa kina. Kwa mfano kama umewahi kuwa kwneye hatari kama kukimbizwa na mnyama kama mbwa utakua umeona unapata nguvu nyingi hata za kuruka ukuta ambao kwa kawaida huwezi kuuruka, hii ndiyo kazi ya ubongo huu. Kwa kiingereza wanasema FIGHT-OR-FRIGHT.
Sehemu ya pili ni ubongo wa kati, ambao una tabia za mnyama. Hii ni sehemu ya ubongo ambayo imebeba hisia zote za mtu. Hisia za upendo, furaha, huzuni, hasira, maombolezo, wivu na hata raha zipo kwenye sehemu hii ya ubongo. Sehemu hii ya ubongo ndiyo inatusukuma kufanya vitu vinavyotupa hisia nzuri na kutuepusha na vitu vinavyoleta hisia mbaya.
[19/06/2016 01:24] Violeth: Sehemu ya tatu ni ubongo wa juu ambao una tabia za utu. Huu ndio ubongo ambao unatutofautisha sisi binadamu na viumbe wengine wote. Huu ndiyo ubongo ambao unafikiri kwa kina kwenye kila jambo tunalofanya au linalotokea. Huu ndio ubongo ambao unatunza kumbukumbu. Ubongo huu unakusanya taarifa kutoka kwenye sehemu nyingine za ubongo na kufanya maamuzi sahihi.
4. kwa bahati mbaya sana, watu wengi wamekuwa wakifanya maamuzi kwa kuongozwa na ubongo wa chini na ubongo wa kati. Ni mara chache sana watu wanaweza kuutumia ubongo wa juu vizuri na kufanya maamuzi bora. Maamuzi mengi yanayofanywa na ubongo wa chini na wa kati ni maamuzi ambayo yana faida ya muda mfupi lakini kwa muda mrefu yana hasara kwao. Mfano ni mtu ambaye anabaka, hapa anauridhisha ubongo wa kati ambao utapata raha, lakini angetumia ubongo wa juu angeona siyo kitu sahihi kwake kufanya.
5. Ili uweze kumshawishi mtu yeyote, hakikisha unaongea naye akiwa kwenye ubongo wa juu. Kama mtu hayupo kwenye ubongo wa juu, hakuna kitu unachoweza kumwambia akakusikia na kukuelewa. Haijalishi utatumia mbinu bora kiasi gani, kama mtu hayupo kwenye ubongo wa juu, unapoteza muda wako.
Hii ndiyo maana ni vigumu sana kumshauri mtu ambaye ana hasira, au aa furaha au yupo katikati ya hisia kali za mapenzi. Kuweza kumshawishi mtu mtoe kwanza kwenye ubongo wa kati na wa chini na mpeleke kwenye ubongo wa juu ambapo anaweza kufikiri sawasawa.
6. Adui wa kwanza wa wewe kuwashawishi wengine ni wewe mwenyewe. Ili uweze kuwashawishi wengine ni lazima wewe ushawishike kwanza. Ni lazima wewe ukubaliane na kile unachotaka wengine wafanye au wakupe. Ni lazima uweze kujidhibiti mwenyewe ili kuweza kuwashawishi wengine kuchukua hatua ambayo unajua ni muhimu kwao.
7. Ondoa chujio ambalo tayari unalo. Kila mmoja wetu ana chujio ambalo anatumia kuwachuja wengine kwa kadiri wanavyoonekana au walivyowazoea. Hivyo tunawapanga watu kwenye makundi kwa kufikiri tunawajua sana. Ili kuweza kuwa na ushawishi kwa wengine kwanza ondoa chujio hili na mwendee kila mtu bila ya kumhukumu, kuwa tayari kujifunza zaidi kutoka kwake. Usimweke mtu kwenye upande wowote, badala yake msikilize yeye kama yeye na hapa utaona njia bora za kuweza kumshawishi.
8. Kila kitu ambacho mtu anafanya, kuna sababu inayomsukuma kufanya. Hakuna mtu anayefanya kitu kwa ajali au kwa bahati mbaya pekee. Hivyo unapokutana na tatizo au changamoto kutoka kwa wengine, jua kuna kitu kimewasukuma kufanya walichofanya. Ili uweze kuwashawishi watu, jua ni kitu gani kinawasukuma wafanye kile ambacho wanafanya sasa na ni jinsi gani unaweza kuwafanya kuacha wanachofanya sasa na wafanye kile ambacho unawashawishi wafanye.
9. Mfanye mtu ajisikie ameeleweka. Ni lazima umwelewe mtu kabla hujataka kumshawishi afanye chochote unachotaka afanye. Jaribu kuvaa viatu vyake na mweleze wazi ya kwamba unaelewa kwa nini yupo pale alipo sasa. Na hata kama anafanya kitu ambacho anakosea, mwelewe kwamba kuna kitu kinasababisha yeye afanye hivyo. Usione kwamba yeye hayupo sahihi na kumweleza hivyo, ukienda kwa njia hiyo atakachofanya ni kujitetea na hutaweza kumshawishi kwa njia yoyote ile. Mwelewe mtu na atafunguka kwako.
10. Kama unataka wengine wajali kuhusu wewe, anza kujali kuhusu wao kwanza. Moja ya njia muhimu za kuweza kuwashawishi watu ni kuwafanya wavutiwe na wewe, wajali kuhusu wewe na hivyo wawe tayari kufanya kile ambacho unawaambia wafanye. Lakini hii haitakuja kwa wewe kukazana watu wavutiwe na wewe na wajali kuhusu wewe. Badala yake inakuja pale unapoanza kujali kuhusu wengine, na unapovutiwa na wengine.
Hivyo unapokutana na watu, usitumie nafasi hiyo kujisifia zaidi wewe, badala yake tumia nafasi hiyo kutaka kuwajua zaidi. Jua ni mambo gani wanafanya, changamoto gani wanapitia, yapi wameweza kukamilisha. Kadiri unavyojali kuhusu wao wanaanza kufunguka kwako na watakuwa tayari kufanya kile unachotaka wafanye.
[19/06/2016 01:25] Violeth: 11. Wafanye wengine wajione ni wa thamani. Hii ni mbinu muhimu sana unayotakiwa kuwa nayo kama unataka kuwashawishi watu kuchukua hatua fulani. Hakuna kitu ambacho mtu anapenda kama kuona amethaminiwa. Hii ndiyo maana watu wanapenda kuitwa mheshimiwa, bosi, mtaalamu, bingwa, na majina mengine yanayoonesha sifa za watu. Mfanye mtu aone ana mchango mkubwa kwenye kile anachofanya na kile unachotaka afanye ataweka mchango mkubwa pia. Kuwafanya watu wa thamani ni zawadi kubwa sana unayoweza kuwapa.
12. Epuka kueleweka tofauti na unavyotaka ueleweke. Katika harakati zako za kuwashawishi wengine, unaweza kuwa unatoa picha ya kinyume kabisa na kile ulichokuwa unataka kutoa wewe. Kwa mfano unataka watu wakuone wewe ni mwenye husara lakini kwao unaonekana ni mpumbavu. Au unataka wakuone ni mwaminifu ila wao wanakuona ni tapeli. Hali hii huwa inatokana na mtu kutokujiandaa vizuri na kutosikiliza wale ambao anataka kuwashawishi. Unahitaji kuwafuatilia kwa makini watu na kuona wanapokeaje kile ambacho unawapatia.
13. Kuna vitu vitatu ambavyo vinawasukuma watu kuchukua hatua, ukiweza kuvitumia vizuri vitu hivi utaweza kuwashawishi watu iwe ni kwenye kazi, biashara na hata kwenye familia.
Kitu cha kwanza ni mapenzi, hamu au shauku. Watu wapo tayari kufanya kile ambacho wanapenda kufanya na wana shauku kubwa ya kukifanya. Hivyo angalia ni kitu gani watu wanapenda na kitumie katika ushawishi wako.
Kitu cha pili ni hamasa. Watu wanapokuwa na hamasa wanakuwa tayari kuchukua hatua kwenye jambo lolote ambalo wanalipenda. Wafanye watu wahamasike kwenye kile ambacho unataka wafanye.
Kitu cha tatu ni fahari, watu wanaona ufahari pale wanapoona wamekuwa na mchango kwenye jambo fulani. Watu wanapoona kile walichofanya kina mchango kwa wengine wanafarijika sana.
Tumia vitu hivi vitatu kwa pamoja na utaweza kuwashawishi watu kuchukua hatua.
14. Uaminifu ni muhimu sana katika kuwashawishi wengine. Huwezi kuwashawishi watu kama hawakuamini na watu hawawezi kukuamini kama husemi ukweli na kutekeleza kile unachoahidi. Usiwe na haraka kwenye ushawishi wako, badala yake jenga mahusiano yenye uaminifu, kadiri watu wanavyokuamini, kutokana na matendo yako na siyo maneno tu, ndivyo wanavyokuwa tayari kukubaliana na wewe.
EPUKA WATU HAWA WA AINA TANO.
Japokuwa lengo la kitabu hiki ni kukupa mbinu za kuweza kuwashawishi watu, kuweza kuwafanya wakubaliane na wewe, kuna watu ambao hawashawishiki na wala hawawezi kukubaliana na wewe kwa lolote. Hawa ni watu ambao ni sumu kali na njia pekee kwako ni kuwaepuka haraka sana. Watu hawa wanajiangalia wao wenyewe sana na hivyo hawawezi kuwa tayari kufanya kitu ambacho kitawanufaisha wengine. Watu hawa wanaongozwa zaidi na ubongo wa chini na wa kati. Watu hao wa aina tano ni kama ifuatavyo;
15. AINA YA KWANZA; Watu ambao ni wahitaji na wategemezi kwako moja kwa moja (needy people). Hawa ni watu wazima, wenye nguvu zao na akili zao lakini wanakuchagua wewe ndiyo ubebe matatizo yao. Wanakuambia wazi kabisa bila ya wewe wao hawawezi kuishi na hivyo wanakutegemea kwa kila kitu. Hata maamuzi madogo ambayo wangeweza kufanya wenyewe hawafanyi mpaka wakusubiri wewe. 
Kama ingekuwa hivi tu wala isingekuwa shida, ila tatizo kubwa la watu hawa ni kwamba wanapenda kulalamika na watakulalamikia kwa kila kitu. Hata uwasaidie kiasi gani, ukikosea kidogo watakulalamikia kwamba umeharibu siku yao au maisha yao. Watataka wewe uache kila unachofanya ushughulikie matatizo yao na ukishindwa kufanya hivi watakulaumu kwamba huwajali.
Hawa ni watu ambao dakika moja watakuambia wewe ndiyo msaada mkubwa kao, na dakika inayofuata watakuambia wewe ndiyo umeharibu maisha yao.
Suluhisho; wakimbie haraka sana watu hawa, kaa nao mbali maana huwezi kuwasaidia kwa lolote. Haijalishi ni ndugu, rafiki au mtu gani, kama amekuwa na tabia hii na ukamweleza lakini habadiliki, kimbia haraka sana.
[19/06/2016 01:27] Violeth: 16. AINA YA PILI; Watu ambao ni waonevu (bullies). Katika maisha yako utakutana na watu ambao ni waonevu, na watakuonea sana. Hawa ni watu ambao wanataka wewe ufanye kile ambacho wanataka wao iwe unataka au hutaki. Hawajali kuhusu wewe wanachojali ni wao wenyewe. Na hawa watakuja wengi kuanzia ndugu, wenza, waajiri na hata washirika kwenye biashara.
Watu ambao ni waonevu wana tabia moja, huwa wanaenda kwa wale watu ambao wanaonekana ni wanyonge. Hivyo njia ya kuwaepuka hawa ni kukataa kuwa mnyonge. Usikubaliane kabisa na kile ambacho watu wanakulazimisha kufanya, hata kama ni mtu gani. Na waambie wazi kwamba hukubaliani na hilo na wakiona wewe ni mgumu watahamia kwa wengine. Kama ni mwajiri anakuwa mwonevu kwako, tafuta kazi nyingine.
17. AINA YA TATU; Watu ambao ni wapokeaji na wachukuaji tu(TAKERS). Hawa ni watu ambao wanajiangalia wao wenyewe tu, kila mara wanakuja kwako na shida ambayo wanataka uwasaidie na wanalalamika sana. Lakini siku wewe una shida ukiwaendea wana kila sababu ya kwa nini hawawezi kukusaidia. Watu hawa wanaona kama wao ndio wanastahili zaidi ya wengine. Watu hawa ni hatari sana kwako kwani wanaweza kuharibu mipango yako na ratiba zako kwa jinsi wanavyokuja na shida zao.
Njia ya kuondokana na watu hawa ni kuwa na kitu ambacho unataka wakufanyie. Pale anapokuja na kitu unataka umsaidie, mwambie sawa nitafanya hivyo ila na mimi nilikuwa naomba unisaidie hiki, (mwambie kitu ambacho unajua kabisa kipo ndani ya uwezo wake), atakimbia na hutamwona tena.
18. AINA YA NNE; Watu ambao wanajijali na kujisifia wao tu (NARCISSISTS). Hawa ni watu ambao wanafikiri duniani wao pekee ndiyo muhimu. Watu hawa huzungumzia zaidi mafanikio yao na kuona wengine kama hawajui wanachokifanya. Watu hawa ukiongea nao wanataka watawale mazungumzo kila unachowaambia wanakuonesha ni jinsi gani wao ni bora kuliko wewe. Watu hawa hawana shida na wewe ila pia hawajali chochote kuhusu wewe. Wanajiangalia wao tu. Waepuke watu hawa kwa kukaa nao mbali, kwa sababu hakuna namna unayoweza kuwashawishi, kwa sababu hawataki kusikia chochote kuhusu wewe, wanataka uwasikilize wao tu na kuwasifia.
19. AINA YA TANO; Watu ambao wana matatizo ya kisaikolojia, au ugonjwa wa akili (PSYCHOPATH). Hawa ni watu ambao hawana hisia zozote zile, wanachoangalia wao ni kile ambacho wanakitaka tu. Hawajui kama wanaumiza wengine na wala hawajali kama wanachotaka kitakuwa kibaya kwa wengine. Kwa tabia hizi watu hawa huwa na mafanikio makubwa kifedha na kikazi au kibiashara lakini kimaisha wanashindwa kwenda vizuri na wengine.  Unapokutana na watu wa aina hii kimbia haraka sana, usitake hata kujadiliana nao, maana wanapokuangalia hawaoni kingine bali ni jinsi gani watanufaika kupitia wewe hata kama wewe utaumia.
Waepuke watu hao wa ina tano na hakikisha wewe mwenyewe haupo katika moja ya aina hizo tano za watu. Kwa sababu badala ya kuwashawishi watu utakuwa unawafukuza kabisa.
20. Katika mipango yako ya kuwashawishi wengine kuwa makini sana usivuke mstari na kuwa mnyonyaji na mkandamizaji. Kuna tofauti ndogo sana kati ya ushawishi na ukandamizaji. Ushawishi ni pale ambapo unawawezesha watu kuchukua hatua au kufanya kitu ambacho kina manufaa kwao. Ukandamizaji ni pale ambapo unawawezesha watu kufanya kitu ambacho kina manufaa kwako ila kwao hakina manufaa au kinawaumiza kabisa. Kuna watu ambao wanaweza kutumia maneno yao vizuri na kuwakandamiza wengine, usiingie kwneye kundi hili.
Ni imani yangu kwamba umejifunza njia za kuongeza ushawishi wako kwa wengine na pia umejua yapi ya kuepuka.
Kama unavyojua, mambo haya yatakusaidia kama utayafanyia kazi.  Hivyo yafanyie kazi.
Kwa kupata vitabu vizuri vya kujisomea kwa lugha ya Kiswahili tembelea MOBILE UNIVERSUTY, www.mobileuniversity.ac.tz Vitabu ni hazina, kila siku jifunze na fanyia kazi yale unayojifunza.

UNACHO TAKIWA KUFANYA UNAPOANZISHA BIASHARA

UNACHOTAKIWA KUFANYA PALE UNAPOANZISHA BIASHARA

Najua nazungumza na mabilionea wakubwa, kama si mabilionea wa sasa, basi ni mabilionea wa baadaye. Wewe ni bilionea, nakutamkia hili na unatakiwa kuamini pasipo kujali kwamba kwenye akaunti una shilingi elfu moja au chini ya hapo, unachotakiwa kuamini kwamba wewe ni bilionea.

Inawezekana umeanzisha biashara yako, kitu cha ajabu kabisa, fedha hazikai, kila ukipata leo, kesho hazipo, ili kuendesha biashara yako inakupasa kukopa sehemu, ni kweli ulipata faida, ila kwa nini ukope? Kopa wakati ukitafuta mtaji, ila kama umeshafanya biashara na faida ukapata, kwa nini ukope? Kwa nini usitumie faida uliyoipata kukuinua hapo ulipo?

Wengi wanakutana na hali hiyo, si wewe tu, hata mimi nilishawahi kukutana nayo, na si sisi tu, amini hata mabilionea wakubwa walishawahi kukutana na hali hiyo. Hivi unajua ni mabilionea wangapi waliwahi kufilisika? Unamjua Muitaliano Enzo Ferrari? Alipata fedha, akafilisika, akagundua alipofanya makosa, akatafuta tena, akazipata.

Wewe kama binadamu wengine, unaweza kupata fedha na kufilisika, hapa siwazungumzii wakina Bakhresa, Mengi na wengineo, nakuzungumzia wewe mwenye biashara ndogo, nataka biashara yako ikue, utoke hapo ulipo na usogee mbele zaidi, ufanikiwe na siku moja uitwe bilionea Omari, Selemani, John, Hamisi, Sara, Anna, Peter au jina lolote ulilokuwa nalo.

Hizi ni baadhi ya njia ambazo zinaweza kukusaidia kufikia ubilionea japokuwa una biashara ndogo au kipato kidogo.

1. WEKA MALENGO: Kitu cha kwanza unachotakiwa kufanya kama mfanyabiashara ni kuweka malengo. Hebu chukua karatasi, andika malengo yako na kuyafanyia kazi. Kumbuka wewe ni bilionea, usiweke malengo ambayo unadhani kwamba pia ua utayafikia, ukiyaandika hayo, jua hautotoa nguvu kubwa kupambana ili uyafikie malengo hayo. Kama una mtaji mdogo, weka malengo makubwa ya kufanikiwa, unapoweka malengo makubwa zaidi ya ulichonacho kitakufanya ujitoe zaidi, uongeze juhudi ili kufikia kile unachokiwazia.

Mfano wewe ni mfanyabiashara mdogo, ukaweka lengo kwamba mpaka mwaka kesho lazima uanzishe biashara ya kuuza mahindi mitaani. Sawa, si vibaya lakini ulitakiwa kuweka malengo ya biashara kubwa zaidi. Kwa fedha hizohizo ulizokuwa nazo, unaweza kuanzisha biashara ya mahindi, ukijiwekea hivyo, jua kwamba unayachelewesha mafanikio yako. Ninataka ujitume kwa nguvu zote, ukiweka yale malengo makubwa, utajiona huwezi kufika lakini ndiyo yatakayokufanya kupambana zaidi, hutolala, utapambana usiku na mchana ila ukiweka lengo dogo, utasema subiri upumzike kwani lengo hilo litakuja hata kama hutojitoa, hivyo ili ufanikiwe, jiwekee lengo kubwa na hakika utapiga hatua.

Mfano mzuri mimi. Sikuwa na fedha kipindi cha nyuma, ishu ya kuanzisha magazeti ilihitaji msingi mkubwa sana, ila sikutaka kukwepa lengo langu la kufanya hivyo. Ningeweza kusema niuze machungwa mitaani, kweli ningeuza, lakini kwa nini niweke lengo dogo? Je ningejitoa zaidi? Ili nijitoe, ili nifanye kazi usiku na mchana ilikuwa ni lazima niweke lengo kubwa, nikaweka, nikajitoa na kufanikiwa. Kama Shigongo, yule mtoto masikini ameweza, vipi kuhusu wewe?

2. USIOGOPE KUFELI: Ndiyo! Kuna watu waoga sana, wanaogopa kufanya biashara fulani kubwa kwa kuwa wanaogopa kuanguka. Rafiki yangu, kuanguka ni sehemu moja ya maisha, ili usonge mbele ni lazima uanguke. Huwezi kujua kuendesha baiskeli kama hujaanguka, ni lazima uanguke ili ujue, iko hivyo.

Mtoto anapoanza kutembea, kuna kipindi anaanguka, mbona yeye hakati tamaa na kusema kwamba kuanzia leo hatembei tena kisa ameanguka? Akianguka, hunyanyuka na kutembea tena, akianguka anajaribu tena.

Wewe kama mfanyabiashara mdogo au mkubwa, jifanye mtoto, usiogope kufeli, ili usonge mbele, ni lazima ufeli, huwezi kuwa mshindi siku zote, kuna kipindi unashindwa, ukishindwa, unakaa chini na kuwaza umeshindwa wapi, unajipanga na kurudi tena kwenye gemu.

Kama ningekuwa naogopa kufeli, nakwambia ukweli kwamba nisingekuwa hapa, labda leo ningekuwa mtaani tu nafanya biashara ndogondogo, kuogopa kufeli kungenifanya niwe kulekule nilipokuwa nyuma. Ili ujifunze, ili upige hatua ni lazima ufeli, ukifeli, unajifunza na kusonga mbele.

3. WEKA UMAKINI NA FEDHA ZAKO: Siku zote nimekuwa nikiwaambia watu, si vizuri kutumia kiasi kikubwa cha fedha zaidi ya unachoingiza. Mwingine ana biashara inaingiza elfu ishirini kwa siku, ila anataka kufanya matumizi yasiyokuwa na faida kwa kutumia elfu thelathini. Ndugu yangu! Huwezi kuishi kwa maisha haya halafu ukaja kufanikiwa. Unatakiwa kuwa makini na fedha zako.

Mwingine anasema, nimepata faida nyingi, acha nikale bata! Ndugu zangu, bata haziishi, kila siku zinaongezeka, baa hazifungwi, umezikuta na utaziacha, kumbi za starehe kila siku zinafunguliwa mpya.

Ithamini pesa yako, hata kama ni shilingi hamsini, ithamini. Unapokuwa na elfu moja, inayokamilisha hela hiyo ni shilingi hamsini, kama ukiwa na 950, huwezi kupata 1000 kama huna hamsini, kwa hiyo kwenye maisha yako ya kibiashara, hata shilingi 50 ni muhimu mno kwako.

Usiipuuzie fedha yoyote ile, panga matumizi yako ya kawaida, si muhimu sana kunywa soda kama huna sababu ya kufanya hivyo! Hakuna umuhimu wa kula chipsi kuku kama hakuna umuhimu wa kufanya hivyo! Kwani usipokula chipsi kuku utakufa? Kama una kiasi kidogo cha fedha basi hata matumizi ya fedha yako hakikisha yanakuwa madogo na si makubwa zaidi ya kile ulichokipata.

4. JENGA URAFIKI NA WENYE FEDHA: Hapa simaanishi kwamba wasiokuwa na fedha inabidi watengwe, hapana! Ila unatakiwa kuwa makini, ni vizuri kutengeneza marafiki wapya lakini inabidi uwe makini. Kabla ya kuwa nilivyo niliwahi kuwasikia watu wakisema unapoanza kufanikiwa unabadilika, nilipinga lakini nikaja kuona inawezekana.

Unapokuwa umefika hatua fulani, automatic unaanza kutafuta watu ambao wanaweza kukuvusha kutoka hapo ulipo, watu wenye uwezo wa kukufanya kufanikiwa zaidi. Kumbuka shuleni kwenu, ni wanafunzi wangapi waliokuwa na akili walikuwa marafiki wao kwa wao? Kwani hawakuwa marafiki zako pia, walikuwa marafiki zako ila wenyewe wakawa beneti, ipo hivyo.

Unapopata fedha, unapofanikiwa, jaribu kutengeneza ukaribu na watu waliofanikiwa, usiwaache wale wengine, kuwa nao ila usiwe nao beneti kupindukia, kama unaona mtu haeleweki, hana hamasa ya kukufanya kufanikiwa, kwa nini uwe naye beneti? Muache awe rafiki wa kupiga naye stori dakika kumi na kuondoka.

Unapokuwa siriazi kutafuta fedha, huna budi kuwatafuta waliofanikiwa, wakufundishe kwa nini wapo hapo, walipitia nyanja zipi mpaka kufanikiwa hivyo? Ni lazima ujifunze kupitia wao na hakika utafanikiwa.

5. USICHANGANYE BIASHARA NA URAFIKI/NDUGU: Ndiyo! Wengi tunafeli hapa. Tunapopata nafasi ya kufanya biashara, wengi tunakosa kufanikiwa kwa sababu tu tumechanganya urafiki katika biashara. Biashara ndogo lakini bado unataka kukopesha, tena kwa watu ambao huna uhakika kama watakulipa.

Unapoanzisha biashara, wengi watakuja kukopa na si kununua, hebu jiulize, wakati hujaanzisha hiyo biashara, mbona hawakuwa wakienda kukopa sehemu nyingine? Jua sisi binadamu tuna makusudi, tunapomuona mtu ameanzisha biashara, mara nyingi tunataka kumuangusha chini ili tumcheke, tumdhihaki kwamba kiko wapi sasa! Unatakiwa kuwa makini sana, huu si muda wa kupeleka urafiki na undugu katika biashara. Unapoanzisha biashara na ikatokea umemuajiri ndugu yako, mwambie wazi kwamba upo kama mfanyabiashara na si kama ndugu, anapofanya makosa, mchukulie hatua kama unavyomchukulia mtu baki, ukimuacha kwa kuogopa lawama, huyohuyo baadaye atakuja kukucheka.

Unapoona una hamu ya kula chipsi, na wewe unaifanya biashara hiyo ya chipsi, nunua chipsi zako, si kwamba ni zako basi na wewe ule bure. Najua ni ngumu kwa watu wengine lakini inabidi ufanye hivyo ili kuifanya biashara yako isimame.
Leo unapouza chipsi na kula bure, amini kwamba kesho utataka uongeze na chipsi yai, keshokutwa chipsi samaki, sasa ukifanya hivyo, hutofanikiwa kwa hiyo ni lazima hata wewe mwenyewe ujidai.

Sina mengi, ila tukutane muda mwingine kwa makala nyingine ya ujasiriamali. Kumbuka, wewe ni bilionea, fanya mambo kama bilionea.

SHARE, LIKE kadiri uwezavyo ili na marafiki zako wajifunze.

MUNGU AKUBARIKI.

FAIDA ZA BIASHARA YA MTANDAO

WATU WOTE WA NAPENDA KUISHI MAISHA MAZURI HIVYO FUATILIA KWA KINA

FAIDA 10 ZA KUFANYA BIASHARA YA MTANDAO

Biashara ya mtandao ni moja ya biashara zinazokua kwa kasi kubwa zaidi katika karne tuliyo nayo sasa. Imeonekana kuwa makampuni yanayofanya biashara hizi yana tabia ya kukua kwa kasi sana na kudumisha ukuaji huo kwa muda mrefu zaidi kuliko makampuni ya biashara za kawaida.
Hadi kufikia 2011, biashara za mtandao zilikaridiwa kufikia kuwa na thamani dola bilioni 100 zikiwa zinatengeneza faida kubwa sana. Haikushangaza kumsikia tajiri mkubwa duniani, Bill Gates, anayemiki kampuni ya software za kompyuta akisema kuwa kama ataruhusiwa kuanza upya biashara, atafanya biashara ya mtandao (network marketing). Katika mada hii tutazizungumzia faida za kufanya biashara hizi za mtandao.
Lakini kabla ya kuanza kuziorodhesha faida hizo tupate maneno machache kuhusu tabia ya biashara hii. Watu wengi huchukulia kwamba biashara hizi ni kimbilio baada ya kushindwa vitu vingine. Napenda kuwashauri kuwa hizi ni biashara kama nyingine zo zote, zinahitaji uwekezaji wa muda, nguvu na pengine pesa. Zina tabia tofauti kidogo na biashara zingine au kazi nyingine za ajira. Wakati hazihitaji mtu kuwa na cheti cha masomo, zinahitaji mwanachama
kuwa na tabia tofauti kidogo na ya mtu aliyezoea kuajiriwa. Hizi ni biashara ambazo mtu anayeshiriki atakuwa mwamuzi wa kila jambo linalohusu biashara yake, akishaanza kufanya biashara hii hakutakuwepo na mtu wa kumsukuma.
Kwa hiyo, zinahitaji mtu awe na uwezo wa kuwa na maamuzi sahihi na kufanya kazi kwa kujipangia mwenyewe. Watu waliofanikwa mapema na kwa kiwango cha juu ni wale waliokuwa na morali ya juu, waliofanya kazi bila kupumzika wakiwa wamejiwekea malengo yao. Hizi ni biashara ambazo unatakiwa kila wakati uzifikirie na kufanya jambo fulani kusogeza gurudumu lako mbele. Unatakiwa kujifunza sana kutoka kwa wale waliokutangulia na wengine wengi
waliokwisha fanikiwa katika biashara hizi.
Kwa vile ni biashara ambazo hazileti utajiri ghafla, zinahitaji uvumilivu wa hali ya juu mwanzoni na kusimama kwenye malengo uliyojiwekea bila kuyumba. Zina tabia ya kuanza kuonyesha matunda taratibu na kuongeza kasi kadiri unavyopanda ngazi kwenye kampuni yako. Ukifika juu, uzito wa kazi hupungua na unaanza kuishi kwa mtindo wa maisha waishio matajiri na watu walio maarufu.
Sasa tuone ni faida gani zinapatikana kutokana na kufanya biashara hizi za mtandao. Kuna faida nyingi sana za kufanya biashara ya mtandao, lakini katika ukurasa huu tumechagua na kuelezea faida 10 tu:
Hii ndio faida kubwa kuliko zote na ndiyo maana hapa nimeiweka kuwa ya kwanza. Hebu fuatilia kwa nini nasema hivyo…..
Katika siku moja idadi ya saa inaeleweka na huwezi kuibadili. Katika saa hizo za siku moja unatakiwa ufanye kazi ya kukupatia kipato, upate muda wa kulala, upate muda wa kuwa na familia na muda mwingine kwa ajili ya shughuli zako nyingine.
Watu wengi wanatakiwa kuwepo mahali walipoajiriwa kwa saa 8 kwa siku … kwenye kazi ambayo wanaifanya tu hata kama hawaipendi. Kwa kubadilishana na muda wao, waajiri huwalipa kiasi fulani cha pesa kwa kila saa aliyokuwepo kazini au kulingana na idadi fulani ya vitu alivyovizalisha. Hakuna malipo ya zaidi ya hapo. Kipato cha mwajiriwa huyu kimefungwa au kimewekewa ukomo kwa sababu;
Kwanza: Kuna ukomo wa idadi ya saa za kufanya kazi, na
Pili: Kuna ukomo wa idadi ya vitu unavyoweza kuvizalisha wewe peke yako katika muda uliopangiwa.
Kwa upande wa pili, tutazame biashara ya mtandao.
Biashara za mtandao huwalipa wanachama wao kutokana na kazi za wanachama wengine. Kwa hiyo basi, mwanachama ambaye ameweza kuongeza idadi ya wanachama walio chini yake atalipwa zaidi, na kila atakapowaongeza zaidi, atazidi kulipwa zaidi.
Uzuri uliopo hapa ni kuwa unaweza kuongeza idadi ya wanachama chini yako bila kuhitaji kuongeza muda wako wa kufanya kazi. Unaweza kupunguza muda wa kufanya kazi na bado ukaona kipato chako kikiongezeka. Ulipwaji kutokana na watu uliowasajili chini yako na kuwafundisha (leveraged income) ndio unaoifanya kuwa faida ya kwanza kwenye orodha hii.
Kampuni za mtandao zinawapa fursa wanachama wao kupata malipo endelevu kwa kazi walizozifanya mara moja. Karibu kila mmoja wa watu wanaojiunga na biashara hizi huwa amevutiwa na aina hii ya malipo. Wewe kama mwanachama unamsajili mwanachama mara mmoja tu na mtu huyu akiendelea kununua bidhaa na kujenga timu inayofanya kazi vizuri, wewe utaendelea kulipwa tena na tena bila ushiriki wako wa moja kwa moja.
Unaweza kuanza biashara ya mtandao kwa mtaji mdogo sana au kwenye kampuni nyingine bila kuwa na mtaji kabisa. Hakuna tofauti kati ya yule aliyenza na mtaji mdogo na yule aliyeanza na mtaji mkubwa, fursa zenu za kufika mnakotaka zinafanana na kubwa kuliko fursa utakayopata kwenye mifumo mingine ya biashara.
Pamoja na kuwa pengine utaanza biashara yako bila mtaji wo wote, utahitaji kiasi fulanai cha pesa kwa ajili ya uendeshaji wa biashara yako ikiwa ni pamoja na kununua bidhaa, mawasiliano, usafiri, matangazo n.k.
Nchini Tanzania, kuna baba ambaye alianza biashara kwa kutoa kiingilio kidogo kwenye kampuni ya FOREVER LIVING PRODUCTS  (kampuni inayohusu bidhaa za afya ya binadamu)     akiwa hana elimu yeyote hata kusoma ilikuwa shida akiwa anafanya biashara ya kuuza  genge Maeneo ya TANDIKA  Dar es salama TANZANIA pia alikuwa na mgogoro na mmiliki wa nyumba aliyopanga kwani  alikuwa anachelewesha kodi ya nyumba. akaanza kwa kupeleka wagonjwa (wateja wake wa Mbogamboga waliochukua ili kuhifadhi afya zao) kupata maelekezo ya virutubisho kutoka kwenye kampuni hiyo Kisha nao wakavutiwa wanaojiunga chini yake, na kukua taratibu hadi kufikia kupata bonasi nzuri kila mwezi na  akaweza kujengakatika nyumba nzuri kipindi kifupi tu – hakuwa na mtaji zaidi ya pesa ya kiingilio.
Kampuni nyingi za mtandao zinaruhusu wanachama wao kufanya biashara kimataifa. Hili linawezekana kwa kutumia mtandao. Unaweza kumsajili mwanachama kutoka nchi yo yote duniani na ukapata kipato kitakachotokana na kazi anayoifanya mwanachama huyu huko aliko. Kwa hiyo unaweza kujijengea biashara kubwa,
katika nchi tafauti, wewe ukiwa ndani ya nyumba yako.
Biashara za mtandao hazihitaji uwe na uzoefu wa kuuza, wala hazihitaji uwe umepata mafunzo ya biashara. Kuwa na uzoefu huo au mafunzo hayo ni kitu kitakachokusaidia, lakini kila mwanachama anayejiunga na biashara hizi hupewa mafunzo ya kutosha. Mafunzo hayo utayapata kutoka kwenye kampuni au kutoka kwa mtu wa juu
yako (aliyekusajili). Kampuni nyingine hutoa mafunzo ya aina mbali mbali kwa wanachama wao, hutoa mafunzo darasani, CD, DVD, vipeperushi na hata vijitabu vya kujisomea.
Kitu kibaya sana kwenye biashara za aina nyingine ni kukosa uhuru na hasa uhuru wa muda. Kazi nyingi zinakutaka ufanye kazi – saa 9 kwa siku, siku 5 kwa wiki – na unapata kipato kwa kuuuza muda huo kwa wiki. Huwezi kujiamulia ufike kazini saa ngapi. Mwajiri wako ndiye anayekupangia nini cha kufanya na wakati gani ukifanye.
Biashara ya mtandao unakuondolea vikwazo vyote hivi. Kuanzia siku ya kwanza unapoanza biashara ya mtandao, unajipangia ufanye kazi na nani… utakataka ufanye kazi muda gani… na utapenda kufanyia wapi kazi yako.
Una uchaguzi wa namna utakavyopenda kufanya biashara yako: kuongea na watu moja kwa moja; kutumia barua pepe; kutumia simu yako ya mkononi, kuitisha mikutano n.k. Ni biashara yako na utaifanya unavyopendezewa ifanyike.
Moja ya faida kubwa ya biashara za mtandao ni kujiendeleza kibinafsi. Wafanya biashara za mtandao ni viongozi makini. Katika kufanya biashara hizi utajiongea ujuzi mwingi na uzoefu mkubwa katika kuzungumza mbele ya kadamnasi, kutoa ushauri, kufundisha watu na namna ya kuishi na watu.
Kufanya biashara ya mtandao kunakuwezesha kufahamiana na watu wa mikondo mbalimbali ya kimaisha, kujipatia marafiki wapya na kujua mikondo mingine ya kibiashara.
Hakuna kiwango cha mapato unachopangiwa kupata. Katika kazi au biashara nyingine za kawaida kiwango chako cha mshahara kimepangwa na hakiwezi kuwa zaidi kwa elimu na ujuzi ulio nao.
Hivyo sivyo katika biashara za mtandao. Wewe ndiye utakayejipangia kiwango unachopenda kukipata, kampuni haina
pingamizi la namna yo yote kama ilivyo kwenye makampuni ya kawaida.
Ukishapata ujuzi wa kufanya biashara ya mtandao, utapata kipato cho chote kulingana na uvumilivu wako na kujituma kwako katika kuwasaidia wengine.
Maendeleo ya teknolojia yanamwezesha mfanya biashara ya mtandao kufanya shughuli zake po pote alipo. Ukiwa na simu ya kiganjani unaweza kuwasiliana na wateja wako kutoka po pote ulipo.
Ukiwa umeunganishwa kwenye internet, unaweza kuchukua simu yako au lap top yako na ukaendelea kufanya biashara zako ukiwa safarini, ukiwa kwenye mapumziko, ukiwa umekwenda kuwaona ndugu walio kwenye mji mwingine na hata ukiwa nchi nyingine.
Baadhi ya bidhaa na huduma bora kabisa ulimwenguni hupatikana kwenye makapuni yanayofanya biashara ya mtandao. Bidhaa hizi haziuzwi kwenye maduka ya kawaida, na hata kama zingeuzwa
humo, hakuna mtu ambaye angezitambua. Bidhaa ikiwa ni nzuri na ya kipekee, inahitaji mtu wa kuielezea, jambo ambalo haliwezekani dukani kutokana na uwingi wa bidhaa katika duka hilo.
Ni yule mtu aliyetumia bidhaa au huduma akaipenda, anayeweza kuuelezea uzuri wa bidhaa au huduma hiyo.
Katika mada yetu ya leo tumeona faida 10 zinazopatikana kwa kufanya biashara za mtandao.

SAFARI YA MAFANIKIO

JE,IPI SAFARI YAKO YA MAFANIKIO UMEPANGA KUPITIA MAANA ZIPO NYINGI

IJUE Orodha Mpya Ya Mabilionea; Mambo Kumi Ya Kuzingati Ili Na Wewe Uweze Kuingia Kwenye Orodha Hii Siku Za Baadae.
Jarida maarufu kwa kufuatilia watu matajiri duniani hivi karibuni limetoa orodha mpya ya watu matajiri sana duniani. Katika orodha hii mpya, mmiliki wa kampuni ya Microsoft, Bill Gates amerudi kwenye nafasi ya kwanza na kuwa mtu tajiri kuliko watu wote duniani. Gates ana utajiri wa dola za kimarekani bilioni 79.2
Orodha hii ya 29, inaonesha kwamba duniani kuna jumla ya mabilionea 1826 na kwa mwaka jana tu mabilionea wapya 290 wameingia kwenye orodha hii. Pia vijana hawajaachwa nyuma, kwani mabilikonea 46 wana umri chini ya miaka 40.
Katika orodha hii ya mabilionea, 29 wanatoka Africa na hata hapa Tanzania tunaye bilionea ambaye ni Mohamed Dewji.
Orodha hii ya mabilionea inamengi sana ya kujifunza ambayo yanatuonesha kwamba nafasi hizi sio kwa ajili ya watu wachache tu. Bali kwa yeyote anayetaka kufikia nafasi hizi anaweza na hata anayezifikia hahakikishiwi kuwepo hapo milele.
Leo katika makala hii tutajadili mambo kumi muhimu ya kuzingatia ili na wewe uweze kuingia kwenye orodha hii miaka ijayo. Mimi tayari nina mpango huo na najua hakuna kinachoweza kunizuia, kama na wewe una mpango huu karibu uongeze mbinu zitakazokusaidia. Kama huna mpango huu pia endelea kusoma na unaweza kuuweka au hata usipouweka bado utakuwa umejifunza mambo muhimu yatakayotatua matatizo yako ya kifedha.
SOMA; Kama Unafikiri Huwezi Kuwa Bilionea Soma Hapa Na Uanze Kuelekea Kwenye Ubilionea.
1. Amini kwamba inawezekana wewe kuwa bilionea.
Hatua ya kwanza kabisa ya wewe kuweza kuwa bilionea ni kuamini kwamba inawezekana. Maana kila kitu kwenye maisha kinaanza na imani. Kama unaamini unaweza ni kweli utaweza. Kama unaamini huwezi ni kweli hutaweza na hakuna atakayeweza kukulazimisha.
Kubali sasa kwamba unaweza kuwa bilionea na amua kuwa bilionea hayo mengine utajifunza ndani ya safari.
2. Mshahara hauwezi kukufikisha kwenye ubilionea.
Kama umeajiriwa unaweza kuchukuia hili ila ndio ukweli wenyewe. Mshahara hauwezi kukufikiasha kwenye ubilionea, sahau kabisa ndugu yangu. Niliangalia kwenye orodha hii ya forbes katika mabilionea 1826, 119uh ni wajasiriamali, yaani wametengeneza ubilionea wao wenyewe. 230 wamerithi utajiri wao na 405 wamerithi sehemu ya utajiri wao na wanaufanyia kazi kuukuza zaidi. Moja kwa moja wewe huwezi kurithi ubilionea kwa hiyo umebakiwa na njia moja tu, UJASIRIAMALI.
SOMA; Njia Nne Za Uhakika Za Kufikia Utajiri, Angalizo; Ajira Sio Mojawapo.
3. Chagua kitu kimoja, au vichache vya kufanya.
Ukiangalia orodha hii ya forbes, asilimia kubwa ya mabilionea wanafanya vitu vichache sana. Kwa mfano Bill Gates anamiliki kampuni ya kutengeneza program za kompyuta, Warren Buffet ni mwekezaji, Aliko Dangote yupo kwenye viwanda.
Ni muhimu sana wewe kuchagua kitu kimoja au vichache unavyopenda kufanya na uvifanyie kazi kwa juhudi na maarifa ili uweze kufikia mafanikio makubwa na utajiri.
4. Usichukie mabilionea.
Baada ya orodha hii kutoka, vyombo mbalimbali vya habari viliweka kwenye mitandao yao ya kijamii na wananchi wakaanza kutoa maoni yao. Wengi walikuwa wanatoa maoni ambayo ni ya hasira dhidi ya mabilionea hawa. Wengi walisema kwamba ni watu ambao ni wabinafsi, hawajali, wana fedha nyingi wakati watu wengine wanakufa njaa na kadhalika. Huenda na wewe una mawazo kama haya, sasa nakwambia mawazo hayo yanakurudisha nyuma. Kwa kuwachukia mabilionea unajizuia na wewe mwenyewe usiwe bilionea. Mambo mengi yanayosemwakuhusu mabilionea ni ya uongo. Soma namba tano hapo chini.
5. Wasaidie wengine.
Kutoa misaada ni moja ya mambo yatakayokuwezesha kufikia ubilionea. Watu wengi na huenda wewe ni mmoja wao wameaminishwa kwamba mabilionea ni watu ambao wanajali fedha zao tu na hawajali masikini. Lakini tukianza na mtu tajiri kuliko wote duniani, Bill Gates ndio mtoa msaada mkubwa duniani kupitia taasisi yake ya BILL AND MELLINDA GATES FAUNDATION. Taasisi hii imesaidia watu wengi sana huku africa na hata hapa Tanzania inafanya kazi. Unahitaji kutoa sehemu ya utajiri wako kwa watu ambao hawajiwezi na utapata utajiri mwingi zaidi.
Siri ya kupokea ni kutoa.
SOMA; Tumia Siri Hii Moja Kupata Chochote Unachotaka Kwenye Maisha Yako.
6. Fanya kazi kwa juhudi na maarifa.
Tabia ya kutega tega kazi haiwezi kukufikisha kwenye ubilionea. Na kwakuwa tumeshakubaliana kwamba ajira haiwezi kukufikisha kwenye ubilionea, unahitaji uwe mtu wa kujituma sana ili uweze kufanikiwa kwenye ujasiriamali. Unahitaji kujua vizuri kile unachofanya na kukifanya kwa ubora wa hali ya juu sanakuliko watu wengine wote walivyowahi kukifanya hapa duniani.
7. Usiridhike na mafanikio kidogo.
Hii ni sumu kubwa kwa watanzania kufikia ubilionea. Mtu anakuwa na biashara inayompatia faida kubwa kuliko wengine wanaomzunguka anaanza kujiona yeye yuko mbali sana. Anaanza kula starehe, kununua magari ya kifahari ambayo hayahitaji, kununua majumba makubwa ambayo hayamzalishii na vitu vingine vingi vya kujionesha. Sikiliza, hakuna wakati ambao unaweza kusema kwamba mimi ndio nimeshayaweza maisha, mimi nimeshakuwa mshindi, wakati huo utakaokubali hivyo ndio wakati ambao utaanz akuanguka, ndio wakati ambao utaanza kushindwa.
Usiridhike na mafanikio kidogo unayopata, endelea kuboresha zaidi na zaidi.
8. Soma, soma, soma.
Nafikiri hiki ni moja ya vitu ambavyo ni muhimu sana kuliko hata hivyo tulivyojadili hapo juu. Maana hata kama huna sifa tulizojadili hapo juu na hata kama hutaki kuwa nazo kwa kuanza kusoma leo, na kuendelea kusoma kila siku utashangaa unaanza kujijengea sifa hizo.
Siku moja mwanafunzi anayemaliza chuo alimuuliza Warren Buffet ni kitu gani anaweza kufanya ili na yeye awe tajiri sana. Warren Buffet alichukua karatasi na kumuonesha akamwambia, soma karatasi 500 kama hizi kila siku. Warren ni mzee, ana miaka 84 ila asilimia 80 ya muda wake wa kazi anautumia kusoma. Hii inamfanya aone ni kampuni gani zinafanya vizuri na kuweza kuzinunua, kusoma kumempa faid akubwa sana kuliko wengine ambao hawasomi kama yeye.
SOMA; Kama Hutajifunza Chochote Mwaka Huu Basi Jifunze Hiki Kimoja Tu
9. Jiunge na KISIMA CHA MAARIFA.
Hili ni eneo muhimu ambapo utapata nafasi ya kujengewa misingi yote muhimu itakayokuwezesha wewe kuwa bilionea. Utajifunza kuhusu biashara na ujasiriamali, utajifunza kuhusu tabia za mafanikio , utapata uchambuzi wa vitabu mbalimbali ambavyo vitakubadili mtazamo wako na kukuongezea maarifa na kikubwa zaidi utapata nafasi ya kuwa kwenye kundi la wasap ambapo unakutana na watu wengine wanaoelekea kwenye ubilionea kama wewe. Yote hayo ni kwa ada ya tsh elfu 50 tu kwa mwaka. Kujiunga bonyeza maandishi haya KISIMA CHA MAARIFA.
SOMA; Faida Kumi Za Kujisomea Ukiacha Kuongeza Maarifa.
10. Soma sana vitabu mbalimbali  na tafuta connection  na watu  waliofanikiwa pia  ili Kupata mwongozo sahahi.

SAFARI YA MAFANIKIO

JE,IPI SAFARI YAKO YA MAFANIKIO UMEPANGA KUPITIA MAANA ZIPO NYINGI

IJUE Orodha Mpya Ya Mabilionea; Mambo Kumi Ya Kuzingati Ili Na Wewe Uweze Kuingia Kwenye Orodha Hii Siku Za Baadae.
Jarida maarufu kwa kufuatilia watu matajiri duniani hivi karibuni limetoa orodha mpya ya watu matajiri sana duniani. Katika orodha hii mpya, mmiliki wa kampuni ya Microsoft, Bill Gates amerudi kwenye nafasi ya kwanza na kuwa mtu tajiri kuliko watu wote duniani. Gates ana utajiri wa dola za kimarekani bilioni 79.2
Orodha hii ya 29, inaonesha kwamba duniani kuna jumla ya mabilionea 1826 na kwa mwaka jana tu mabilionea wapya 290 wameingia kwenye orodha hii. Pia vijana hawajaachwa nyuma, kwani mabilikonea 46 wana umri chini ya miaka 40.
Katika orodha hii ya mabilionea, 29 wanatoka Africa na hata hapa Tanzania tunaye bilionea ambaye ni Mohamed Dewji.
Orodha hii ya mabilionea inamengi sana ya kujifunza ambayo yanatuonesha kwamba nafasi hizi sio kwa ajili ya watu wachache tu. Bali kwa yeyote anayetaka kufikia nafasi hizi anaweza na hata anayezifikia hahakikishiwi kuwepo hapo milele.
Leo katika makala hii tutajadili mambo kumi muhimu ya kuzingatia ili na wewe uweze kuingia kwenye orodha hii miaka ijayo. Mimi tayari nina mpango huo na najua hakuna kinachoweza kunizuia, kama na wewe una mpango huu karibu uongeze mbinu zitakazokusaidia. Kama huna mpango huu pia endelea kusoma na unaweza kuuweka au hata usipouweka bado utakuwa umejifunza mambo muhimu yatakayotatua matatizo yako ya kifedha.
SOMA; Kama Unafikiri Huwezi Kuwa Bilionea Soma Hapa Na Uanze Kuelekea Kwenye Ubilionea.
1. Amini kwamba inawezekana wewe kuwa bilionea.
Hatua ya kwanza kabisa ya wewe kuweza kuwa bilionea ni kuamini kwamba inawezekana. Maana kila kitu kwenye maisha kinaanza na imani. Kama unaamini unaweza ni kweli utaweza. Kama unaamini huwezi ni kweli hutaweza na hakuna atakayeweza kukulazimisha.
Kubali sasa kwamba unaweza kuwa bilionea na amua kuwa bilionea hayo mengine utajifunza ndani ya safari.
2. Mshahara hauwezi kukufikisha kwenye ubilionea.
Kama umeajiriwa unaweza kuchukuia hili ila ndio ukweli wenyewe. Mshahara hauwezi kukufikiasha kwenye ubilionea, sahau kabisa ndugu yangu. Niliangalia kwenye orodha hii ya forbes katika mabilionea 1826, 119uh ni wajasiriamali, yaani wametengeneza ubilionea wao wenyewe. 230 wamerithi utajiri wao na 405 wamerithi sehemu ya utajiri wao na wanaufanyia kazi kuukuza zaidi. Moja kwa moja wewe huwezi kurithi ubilionea kwa hiyo umebakiwa na njia moja tu, UJASIRIAMALI.
SOMA; Njia Nne Za Uhakika Za Kufikia Utajiri, Angalizo; Ajira Sio Mojawapo.
3. Chagua kitu kimoja, au vichache vya kufanya.
Ukiangalia orodha hii ya forbes, asilimia kubwa ya mabilionea wanafanya vitu vichache sana. Kwa mfano Bill Gates anamiliki kampuni ya kutengeneza program za kompyuta, Warren Buffet ni mwekezaji, Aliko Dangote yupo kwenye viwanda.
Ni muhimu sana wewe kuchagua kitu kimoja au vichache unavyopenda kufanya na uvifanyie kazi kwa juhudi na maarifa ili uweze kufikia mafanikio makubwa na utajiri.
4. Usichukie mabilionea.
Baada ya orodha hii kutoka, vyombo mbalimbali vya habari viliweka kwenye mitandao yao ya kijamii na wananchi wakaanza kutoa maoni yao. Wengi walikuwa wanatoa maoni ambayo ni ya hasira dhidi ya mabilionea hawa. Wengi walisema kwamba ni watu ambao ni wabinafsi, hawajali, wana fedha nyingi wakati watu wengine wanakufa njaa na kadhalika. Huenda na wewe una mawazo kama haya, sasa nakwambia mawazo hayo yanakurudisha nyuma. Kwa kuwachukia mabilionea unajizuia na wewe mwenyewe usiwe bilionea. Mambo mengi yanayosemwakuhusu mabilionea ni ya uongo. Soma namba tano hapo chini.
5. Wasaidie wengine.
Kutoa misaada ni moja ya mambo yatakayokuwezesha kufikia ubilionea. Watu wengi na huenda wewe ni mmoja wao wameaminishwa kwamba mabilionea ni watu ambao wanajali fedha zao tu na hawajali masikini. Lakini tukianza na mtu tajiri kuliko wote duniani, Bill Gates ndio mtoa msaada mkubwa duniani kupitia taasisi yake ya BILL AND MELLINDA GATES FAUNDATION. Taasisi hii imesaidia watu wengi sana huku africa na hata hapa Tanzania inafanya kazi. Unahitaji kutoa sehemu ya utajiri wako kwa watu ambao hawajiwezi na utapata utajiri mwingi zaidi.
Siri ya kupokea ni kutoa.
SOMA; Tumia Siri Hii Moja Kupata Chochote Unachotaka Kwenye Maisha Yako.
6. Fanya kazi kwa juhudi na maarifa.
Tabia ya kutega tega kazi haiwezi kukufikisha kwenye ubilionea. Na kwakuwa tumeshakubaliana kwamba ajira haiwezi kukufikisha kwenye ubilionea, unahitaji uwe mtu wa kujituma sana ili uweze kufanikiwa kwenye ujasiriamali. Unahitaji kujua vizuri kile unachofanya na kukifanya kwa ubora wa hali ya juu sanakuliko watu wengine wote walivyowahi kukifanya hapa duniani.
7. Usiridhike na mafanikio kidogo.
Hii ni sumu kubwa kwa watanzania kufikia ubilionea. Mtu anakuwa na biashara inayompatia faida kubwa kuliko wengine wanaomzunguka anaanza kujiona yeye yuko mbali sana. Anaanza kula starehe, kununua magari ya kifahari ambayo hayahitaji, kununua majumba makubwa ambayo hayamzalishii na vitu vingine vingi vya kujionesha. Sikiliza, hakuna wakati ambao unaweza kusema kwamba mimi ndio nimeshayaweza maisha, mimi nimeshakuwa mshindi, wakati huo utakaokubali hivyo ndio wakati ambao utaanz akuanguka, ndio wakati ambao utaanza kushindwa.
Usiridhike na mafanikio kidogo unayopata, endelea kuboresha zaidi na zaidi.
8. Soma, soma, soma.
Nafikiri hiki ni moja ya vitu ambavyo ni muhimu sana kuliko hata hivyo tulivyojadili hapo juu. Maana hata kama huna sifa tulizojadili hapo juu na hata kama hutaki kuwa nazo kwa kuanza kusoma leo, na kuendelea kusoma kila siku utashangaa unaanza kujijengea sifa hizo.
Siku moja mwanafunzi anayemaliza chuo alimuuliza Warren Buffet ni kitu gani anaweza kufanya ili na yeye awe tajiri sana. Warren Buffet alichukua karatasi na kumuonesha akamwambia, soma karatasi 500 kama hizi kila siku. Warren ni mzee, ana miaka 84 ila asilimia 80 ya muda wake wa kazi anautumia kusoma. Hii inamfanya aone ni kampuni gani zinafanya vizuri na kuweza kuzinunua, kusoma kumempa faid akubwa sana kuliko wengine ambao hawasomi kama yeye.
SOMA; Kama Hutajifunza Chochote Mwaka Huu Basi Jifunze Hiki Kimoja Tu
9. Jiunge na KISIMA CHA MAARIFA.
Hili ni eneo muhimu ambapo utapata nafasi ya kujengewa misingi yote muhimu itakayokuwezesha wewe kuwa bilionea. Utajifunza kuhusu biashara na ujasiriamali, utajifunza kuhusu tabia za mafanikio , utapata uchambuzi wa vitabu mbalimbali ambavyo vitakubadili mtazamo wako na kukuongezea maarifa na kikubwa zaidi utapata nafasi ya kuwa kwenye kundi la wasap ambapo unakutana na watu wengine wanaoelekea kwenye ubilionea kama wewe. Yote hayo ni kwa ada ya tsh elfu 50 tu kwa mwaka. Kujiunga bonyeza maandishi haya KISIMA CHA MAARIFA.
SOMA; Faida Kumi Za Kujisomea Ukiacha Kuongeza Maarifa.
10. Soma sana vitabu mbalimbali  na tafuta connection  na watu  waliofanikiwa pia  ili Kupata mwongozo sahahi.

BIASHARA YA MTANDAO

WATU WOTE WA NAPENDA KUISHI MAISHA MAZURI HIVYO FUATILIA KWA KINA

FAIDA 10 ZA KUFANYA BIASHARA YA MTANDAO

Biashara ya mtandao ni moja ya biashara zinazokua kwa kasi kubwa zaidi katika karne tuliyo nayo sasa. Imeonekana kuwa makampuni yanayofanya biashara hizi yana tabia ya kukua kwa kasi sana na kudumisha ukuaji huo kwa muda mrefu zaidi kuliko makampuni ya biashara za kawaida.
Hadi kufikia 2011, biashara za mtandao zilikaridiwa kufikia kuwa na thamani dola bilioni 100 zikiwa zinatengeneza faida kubwa sana. Haikushangaza kumsikia tajiri mkubwa duniani, Bill Gates, anayemiki kampuni ya software za kompyuta akisema kuwa kama ataruhusiwa kuanza upya biashara, atafanya biashara ya mtandao (network marketing). Katika mada hii tutazizungumzia faida za kufanya biashara hizi za mtandao.
Lakini kabla ya kuanza kuziorodhesha faida hizo tupate maneno machache kuhusu tabia ya biashara hii. Watu wengi huchukulia kwamba biashara hizi ni kimbilio baada ya kushindwa vitu vingine. Napenda kuwashauri kuwa hizi ni biashara kama nyingine zo zote, zinahitaji uwekezaji wa muda, nguvu na pengine pesa. Zina tabia tofauti kidogo na biashara zingine au kazi nyingine za ajira. Wakati hazihitaji mtu kuwa na cheti cha masomo, zinahitaji mwanachama
kuwa na tabia tofauti kidogo na ya mtu aliyezoea kuajiriwa. Hizi ni biashara ambazo mtu anayeshiriki atakuwa mwamuzi wa kila jambo linalohusu biashara yake, akishaanza kufanya biashara hii hakutakuwepo na mtu wa kumsukuma.
Kwa hiyo, zinahitaji mtu awe na uwezo wa kuwa na maamuzi sahihi na kufanya kazi kwa kujipangia mwenyewe. Watu waliofanikwa mapema na kwa kiwango cha juu ni wale waliokuwa na morali ya juu, waliofanya kazi bila kupumzika wakiwa wamejiwekea malengo yao. Hizi ni biashara ambazo unatakiwa kila wakati uzifikirie na kufanya jambo fulani kusogeza gurudumu lako mbele. Unatakiwa kujifunza sana kutoka kwa wale waliokutangulia na wengine wengi
waliokwisha fanikiwa katika biashara hizi.
Kwa vile ni biashara ambazo hazileti utajiri ghafla, zinahitaji uvumilivu wa hali ya juu mwanzoni na kusimama kwenye malengo uliyojiwekea bila kuyumba. Zina tabia ya kuanza kuonyesha matunda taratibu na kuongeza kasi kadiri unavyopanda ngazi kwenye kampuni yako. Ukifika juu, uzito wa kazi hupungua na unaanza kuishi kwa mtindo wa maisha waishio matajiri na watu walio maarufu.
Sasa tuone ni faida gani zinapatikana kutokana na kufanya biashara hizi za mtandao. Kuna faida nyingi sana za kufanya biashara ya mtandao, lakini katika ukurasa huu tumechagua na kuelezea faida 10 tu:
Hii ndio faida kubwa kuliko zote na ndiyo maana hapa nimeiweka kuwa ya kwanza. Hebu fuatilia kwa nini nasema hivyo…..
Katika siku moja idadi ya saa inaeleweka na huwezi kuibadili. Katika saa hizo za siku moja unatakiwa ufanye kazi ya kukupatia kipato, upate muda wa kulala, upate muda wa kuwa na familia na muda mwingine kwa ajili ya shughuli zako nyingine.
Watu wengi wanatakiwa kuwepo mahali walipoajiriwa kwa saa 8 kwa siku … kwenye kazi ambayo wanaifanya tu hata kama hawaipendi. Kwa kubadilishana na muda wao, waajiri huwalipa kiasi fulani cha pesa kwa kila saa aliyokuwepo kazini au kulingana na idadi fulani ya vitu alivyovizalisha. Hakuna malipo ya zaidi ya hapo. Kipato cha mwajiriwa huyu kimefungwa au kimewekewa ukomo kwa sababu;
Kwanza: Kuna ukomo wa idadi ya saa za kufanya kazi, na
Pili: Kuna ukomo wa idadi ya vitu unavyoweza kuvizalisha wewe peke yako katika muda uliopangiwa.
Kwa upande wa pili, tutazame biashara ya mtandao.
Biashara za mtandao huwalipa wanachama wao kutokana na kazi za wanachama wengine. Kwa hiyo basi, mwanachama ambaye ameweza kuongeza idadi ya wanachama walio chini yake atalipwa zaidi, na kila atakapowaongeza zaidi, atazidi kulipwa zaidi.
Uzuri uliopo hapa ni kuwa unaweza kuongeza idadi ya wanachama chini yako bila kuhitaji kuongeza muda wako wa kufanya kazi. Unaweza kupunguza muda wa kufanya kazi na bado ukaona kipato chako kikiongezeka. Ulipwaji kutokana na watu uliowasajili chini yako na kuwafundisha (leveraged income) ndio unaoifanya kuwa faida ya kwanza kwenye orodha hii.
Kampuni za mtandao zinawapa fursa wanachama wao kupata malipo endelevu kwa kazi walizozifanya mara moja. Karibu kila mmoja wa watu wanaojiunga na biashara hizi huwa amevutiwa na aina hii ya malipo. Wewe kama mwanachama unamsajili mwanachama mara mmoja tu na mtu huyu akiendelea kununua bidhaa na kujenga timu inayofanya kazi vizuri, wewe utaendelea kulipwa tena na tena bila ushiriki wako wa moja kwa moja.
Unaweza kuanza biashara ya mtandao kwa mtaji mdogo sana au kwenye kampuni nyingine bila kuwa na mtaji kabisa. Hakuna tofauti kati ya yule aliyenza na mtaji mdogo na yule aliyeanza na mtaji mkubwa, fursa zenu za kufika mnakotaka zinafanana na kubwa kuliko fursa utakayopata kwenye mifumo mingine ya biashara.
Pamoja na kuwa pengine utaanza biashara yako bila mtaji wo wote, utahitaji kiasi fulanai cha pesa kwa ajili ya uendeshaji wa biashara yako ikiwa ni pamoja na kununua bidhaa, mawasiliano, usafiri, matangazo n.k.
Nchini Tanzania, kuna baba ambaye alianza biashara kwa kutoa kiingilio kidogo kwenye kampuni ya FOREVER LIVING PRODUCTS  (kampuni inayohusu bidhaa za afya ya binadamu)     akiwa hana elimu yeyote hata kusoma ilikuwa shida akiwa anafanya biashara ya kuuza  genge Maeneo ya TANDIKA  Dar es salama TANZANIA pia alikuwa na mgogoro na mmiliki wa nyumba aliyopanga kwani  alikuwa anachelewesha kodi ya nyumba. akaanza kwa kupeleka wagonjwa (wateja wake wa Mbogamboga waliochukua ili kuhifadhi afya zao) kupata maelekezo ya virutubisho kutoka kwenye kampuni hiyo Kisha nao wakavutiwa wanaojiunga chini yake, na kukua taratibu hadi kufikia kupata bonasi nzuri kila mwezi na  akaweza kujengakatika nyumba nzuri kipindi kifupi tu – hakuwa na mtaji zaidi ya pesa ya kiingilio.
Kampuni nyingi za mtandao zinaruhusu wanachama wao kufanya biashara kimataifa. Hili linawezekana kwa kutumia mtandao. Unaweza kumsajili mwanachama kutoka nchi yo yote duniani na ukapata kipato kitakachotokana na kazi anayoifanya mwanachama huyu huko aliko. Kwa hiyo unaweza kujijengea biashara kubwa,
katika nchi tafauti, wewe ukiwa ndani ya nyumba yako.
Biashara za mtandao hazihitaji uwe na uzoefu wa kuuza, wala hazihitaji uwe umepata mafunzo ya biashara. Kuwa na uzoefu huo au mafunzo hayo ni kitu kitakachokusaidia, lakini kila mwanachama anayejiunga na biashara hizi hupewa mafunzo ya kutosha. Mafunzo hayo utayapata kutoka kwenye kampuni au kutoka kwa mtu wa juu
yako (aliyekusajili). Kampuni nyingine hutoa mafunzo ya aina mbali mbali kwa wanachama wao, hutoa mafunzo darasani, CD, DVD, vipeperushi na hata vijitabu vya kujisomea.
Kitu kibaya sana kwenye biashara za aina nyingine ni kukosa uhuru na hasa uhuru wa muda. Kazi nyingi zinakutaka ufanye kazi – saa 9 kwa siku, siku 5 kwa wiki – na unapata kipato kwa kuuuza muda huo kwa wiki. Huwezi kujiamulia ufike kazini saa ngapi. Mwajiri wako ndiye anayekupangia nini cha kufanya na wakati gani ukifanye.
Biashara ya mtandao unakuondolea vikwazo vyote hivi. Kuanzia siku ya kwanza unapoanza biashara ya mtandao, unajipangia ufanye kazi na nani… utakataka ufanye kazi muda gani… na utapenda kufanyia wapi kazi yako.
Una uchaguzi wa namna utakavyopenda kufanya biashara yako: kuongea na watu moja kwa moja; kutumia barua pepe; kutumia simu yako ya mkononi, kuitisha mikutano n.k. Ni biashara yako na utaifanya unavyopendezewa ifanyike.
Moja ya faida kubwa ya biashara za mtandao ni kujiendeleza kibinafsi. Wafanya biashara za mtandao ni viongozi makini. Katika kufanya biashara hizi utajiongea ujuzi mwingi na uzoefu mkubwa katika kuzungumza mbele ya kadamnasi, kutoa ushauri, kufundisha watu na namna ya kuishi na watu.
Kufanya biashara ya mtandao kunakuwezesha kufahamiana na watu wa mikondo mbalimbali ya kimaisha, kujipatia marafiki wapya na kujua mikondo mingine ya kibiashara.
Hakuna kiwango cha mapato unachopangiwa kupata. Katika kazi au biashara nyingine za kawaida kiwango chako cha mshahara kimepangwa na hakiwezi kuwa zaidi kwa elimu na ujuzi ulio nao.
Hivyo sivyo katika biashara za mtandao. Wewe ndiye utakayejipangia kiwango unachopenda kukipata, kampuni haina
pingamizi la namna yo yote kama ilivyo kwenye makampuni ya kawaida.
Ukishapata ujuzi wa kufanya biashara ya mtandao, utapata kipato cho chote kulingana na uvumilivu wako na kujituma kwako katika kuwasaidia wengine.
Maendeleo ya teknolojia yanamwezesha mfanya biashara ya mtandao kufanya shughuli zake po pote alipo. Ukiwa na simu ya kiganjani unaweza kuwasiliana na wateja wako kutoka po pote ulipo.
Ukiwa umeunganishwa kwenye internet, unaweza kuchukua simu yako au lap top yako na ukaendelea kufanya biashara zako ukiwa safarini, ukiwa kwenye mapumziko, ukiwa umekwenda kuwaona ndugu walio kwenye mji mwingine na hata ukiwa nchi nyingine.
Baadhi ya bidhaa na huduma bora kabisa ulimwenguni hupatikana kwenye makapuni yanayofanya biashara ya mtandao. Bidhaa hizi haziuzwi kwenye maduka ya kawaida, na hata kama zingeuzwa
humo, hakuna mtu ambaye angezitambua. Bidhaa ikiwa ni nzuri na ya kipekee, inahitaji mtu wa kuielezea, jambo ambalo haliwezekani dukani kutokana na uwingi wa bidhaa katika duka hilo.
Ni yule mtu aliyetumia bidhaa au huduma akaipenda, anayeweza kuuelezea uzuri wa bidhaa au huduma hiyo.
Katika mada yetu ya leo tumeona faida 10 zinazopatikana kwa kufanya biashara za mtandao.

KUNA NJIA NYINGI ZA MAFANIKIO

MASOMO MATATU

SOMO LA KWANZA.

Ilitokea kipindi cha nyuma kidogo. Nilikuwa katika ukumbi nikimsikiliza mhamasishaji (Motivational speaker). Mhamasishaji alitoa mfukoni noti za shilingi elfu kumi kumi zilizokuwa na jumla ya Tsh laki moja, akauliza, "ni nani miongoni mwenu anataka nimpe hii laki moja?"

Watu wengi waliokuwa mle ukumbini walinyosha mikono, kila mmoja alikuwa akishauti mimi! Mimi!. Nikaanza kushangaa ni nani atakuwa na bahati ya kupewa ile pesa kati ya mamia ya watu waliohudhuria ile semina.

Pia nikajiuliza kwa nini (ambapo bila shaka na baadhi ya wahuzuriaji wengine nao walijiuliza) atoe kitita cha shilingi laki moja kirahisi rahisi hivyo.

Wakati watu wakiendelea kupiga kelele kusema nipe mimi, nipe mimi huku wamenyosha vidole vyao, kutokea nyuma akaibuka msichana mdogo mwenye umri kama miaka 18 hivi, akaenda mbele kule aliko yule speaker akapanda stejini na kuchukua ile laki moja kutoka mkononi mwa yule mhamasishaji.

"Safi sana, msichana! Umefanya vema," alisema yule mhamasishaji. "Wengi wetu tunapenda kukaa tu na kusubiri mambo mazuri yaje yenyewe. Hii haitaweza kuwasaidia hata kidogo, unatakiwa kuinuka na kutafuta mafanikio. Mafanikio hayawezi kuja kama umekaa tu.

Na maisha yetu ndivyo yalivyo, tunaziona fursa nyingi sana zikiwa zimetuzunguka, kila mtu anahitaji mambo mazuri. Ila tatizo hatutaki kusimama na kuzifuata hzo fursa. Simama sasa na ufanye kitu, usisubiri mafanikio huku umekaa, kamwe hayatakuja. Usijali kuhusu watu watasema nini. Chukua hatua.

SOMO LA PILI.

Baadae yule Mhamasishaji akatoa tena noti ya shilingi 10000 na akainyanyua ili wote tuione. Nikafikiri anarudia kama mwanzo tena. Lakini akauliza swali jepesi. "Noti hii inathamani gani?" Wahudhuriaji wakajibu "shilingi elfu kumi". "Mko sahihi" akawajibu.

Akaichukua ile noti akaifinyanga finyanga na kuwauliza tena noti ile inathamani ya shilingi ngapi!? "shilingi elfu kumi" wakajibu wale wahudhuriaji!

Akaitupa chini ipe noti, akaikanyaga kanyaga sana, akaichukua na kuuliza tena noti hii ina thamani ya kiasi gani? "Shilingi elfu kumi" wahudhuriaji walijibu vilevile.

Mhamasishaji akawaambia nataka muweka katika akili yenu hili, "mtu hata aichakaze, aikunje kunje na kuikanyaga noti ya fedha, thamani ya noti itabaki pale pale."

"Maisha yetu ndivyo yalivyo, tunatakiwa tuwe kama noti ya shilingi elfu kumi. Ktk maisha kuna kipindi tutasalitiwa, tutakanyagwa, tutaonewa na kupigwa. Ila usiache thamani yako ipotee, kwa sababu mtu amekuumiza tu, hiyo haimaanishi ndio thamani yako imepotea. Wewe ni wa thamani mno jinsi ulivyo. Usiache thamani yako ipotee kwa sababu ya wapumbavu wachache!

SOMO LA MWISHO.

Njia tofauti, jibu moja.
2+5=7
6+1=7
3+4=7
7-0=7
7+0=7
9-2=7
8-1=7

Pointi yangu iko wapi?

Pointi yangu ni kwamba kuna njia nyingi za kufikia mafanikio yako. Mungu hawezi kukufikisha katika mafanikio yako labda kama mama yako, baba yako, marafiki au ndugu walivyofanikiwa, kila mmoja hua na njia ya mafanikio tofauti Mungu aliyompangia.

Unaweza fikia mafanikio yako aidha kwa kuongeza watu katika maisha yako au kupunguza watu. "kujumlisha na kutoa" marafiki na baadhi ya vitu katika maisha yako kunaweza kusiwe kwa furaha kwa upande wako, ila Mungu ana makusudi yake.

Katika safari yako unaweza ukakumbana na kusalitiwa, kuumizwa kihisia, kuchekwa na kusimangwa! Acha kulia na futa machozi yako kila hali unayopitia ina makusudi yake. Mungu anakutengeneza uwe bora zaidi ya hivyo ulivyo.

Jibu langu ni jepesi tu

TUTAKUA KAMA VILE MUNGU ALIVYOTUPANGIA TUWE!
Mwenyezi Mungu awabariki.

IKUMBUKE NDOTO YAKO

Kuna mambo mawili ambayo kama ukiweza kuyazingatia kuanzia leo basi yatabadilisha kabisa aina ya maisha unayoishi na yatakusaidia kukupa uhakika wa kufanikiwa katika malengo na ndoto ulizonazo maishani mwako.

Moja ni lile ambalo tunajifunza kutokana na maisha ya Anthony Burgess.Alipofikisha miaka 40 Anthony Burgess aligundulika kuwa ana mwaka mmoja tu wa kuishi baada ya madaktari bingwa kugundua kuwa alikuwa na uvimbe mkubwa sana katika ubongo(brain tumor) ambao ulikuwa unazidi kukua kila siku.Mara baada ya kupewa taarifa hii aligundua kuwa hana muda mrefu wa kuishi na mawazo yakaanza kumjia kwani kwa wakati huo alikuwa amefilisika kabisa na hana chochote kile kifedha.Alianza kuwaza jinsi mke wake Lynne atakavyoteseka baada ya yeye kufariki.

Kabla ya kugundulika na tatizo hili Burgess hakuwahi kuwa mwandishi mahiri wa vitabu vya hadithi(novel) lakini siku zote alijua kuwa ana kipaji na uwezo huo ndani yake.Baada ya kutafakari maisha ya mke wake yatakuwaje aliamua kutumia muda wote uliobakia wa mwaka mmoja kabla hajafariki kuandika vitabu ili hata baada ya kufa basi mke wake aendelee kufaidika na mauzo ya vitabu hivyo.Akiwa katika hatua hii hakujua kama vitabu hivyo vitafanikiwa kuuzika lakini hakuwa na chaguo la kufanya kitu kingine.

Burgess anasema “Ilikuwa ni mwezi wa kwanza mwaka 1960” nilipoambiwa rasmi kuwa nina mwaka mmoja tu wa kuishi.Kwa namna isiyo ya kawaida ndani ya mwaka huo mmoja alifanikiwa kuandika vitabu vitano.Cha kushangaza kilichotokea ni kuwa hakufariki kama madaktari walivyotabiri na baada ya hapo alifanikiwa kuandika vitabu zaidi ya 70 kabla hajafariki.

Hili ni jambo la kawaida sana kwa wengi wetu,huwa hatufanyi kitu hadi pale hali inapoonekana haina namna/haina suluhisho lingine.Hii inamanisha kama utalitambua hilo kila siku basi unaweza kufanikiwa kufanya mambo makubwa kila siku.Ubongo wako una nguvu ya kipekee ambayo inaweza kuanza kufanya kazi mara tu utakapotambua kuwa hauna muda wa kutosha.Watu wanaofanikiwa ni wale ambao kila wakati wanajua kuwa muda walionao kufanya mambo ni mchache,kwa sababu hiyo huwa wanajikuta wanaulazimisha ubongo wao kufanya mambo mengi ndani ya muda mfupi.

Kama asingeambiwa kuwa ana mwaka mmoja wa kuishi basi Burgess angekufa na vitabu vyake vyote sabini bila kuviandika.Kuna wengi wataondoka duniani bila kutoa vipaji na uwezo walionao ndani yao,naamini wewe hautakuwa mmoja wa hao watu.Ili leo ichangie katika mafanikio yako ni lazima uiishi kama vile hauna muda wa kutosha-Acha kupoteza muda kwenye mambo yasiyochangia mafanikio yako,acha kuchart mambo yanayopoteza muda wako,acha kusoma vitu vinavyojaza ubongo wako na mambo hasi(negative).

Ili ufanikiwe ni lazima HAMU yako ya mafanikio iwe kubwa kuliko HOFU yako ya kufeli.Siku moja kijana mmoja alimfuata Socrates na akataka amwambie siri ya mafanikio,basi Socrates akamwambia wakutane kesho yake asubuhi mtoni.Asubuhi ilipofika Socrates alimwambia yule kijana waingie ndani ya mto kidogo na ghafla akamchukua na kumtumbukiza kichwa chake ndani ya maji.Akiwa anahangaika kupata hewa Socrates aliendelea kumshikilia kitambo kidogo kisha akamwachia.Baada ya hapo walipotoka nje ya maji Socrates akamuuliza yule kijana-“Wakati nimekuingiza ndani ya maji,ulitamani nini zaidi?” yule kijana akasema-“Hewa”-Socrates akamwambia “kama ukitamani mafanikio kama ulivyohangaika kutafuta hewa wakati uko ndani ya maji basi utafanikiwa,hiyo ndio siri ya mafanikio hakuna siri nyingine ya mafanikio”

Hili ndio jambo la pili unalolihitaji baada ya kuanza kujua kuwa una muda mchache basi lazima uwe na shauku ya mfanikio kama vile unavyokuwa na shauku ya hewa unapokuwa ndani ya maji.Watu wengi huwa wanasema wanataka kufanikiwa lakini ndani kabisa ya mioyo yao shauku yao ya mafanikio bado ni ndogo ukilinganisha na hofu yao ya kufeli.

Utajua kama shauku yako ya mafanikio ni ndogo kama ukifeli mara moja unakata tamaa,utajua kama shauku yako ya mafanikio ni ndogo kama kila siku unasema utaanza kufanya ila hadi leo haujaanza,utajua kama shauku yako ya mafanikio ni ndogo kama maneno ya watu yanakukatisha tamaa kuiishi ndoto yako,utajua kama shauku yako ya mafanikio ni ndogo kama unaweza kuangalia tamthilia kwa lisaa limoja kila siku lakini huwezi kusoma kitabu kwa dakika ishirini kila siku,utajua kama shauku yako ya mafanikio ni ndogo kama unaweza kununua vocha kila wiki ila hauwezi kununua kitabu,jarida,CD ama DVD ya mafunzo fulani.utajua kama hauna shauku ya mafanikio kama unajifunza mambo mengi kila siku lakini hauyafanyii kazi.

Mafanikio katika maisha huwa yanaongozwa na kanuni,kama ukianza leo kuishi kwa kujua kuwa muda wako sio wa kupoteza na pia kuishi kwa shauku ya kiwango cha juu ya mafanikio yako basi sina shaka utafanikiwa.

Kumbuka kuwa Ndoto Yako Inawezekana,

See You At The Top.

USITEGEMEE MSHAHARA TU

UKWELI KUHUSU MSHAHARA.

1. Epuka kugeuza mshahara wako kuwa mali ya ukoo. Kamwe mshahara wako siyo mali ya ukoo. Siku utakapoacha kuufanya mshahara wako mali ya ukoo ndipo siku mshahara huo utakuwa mkubwa! Hapo ndipo mshahara utatosha.

2. Siku utakapokuwa na vyanzo vya mapato zaidi ya mshahara wako ndipo mshahara wako utakapotosha mahitaji yako ya kila mwezi.

3. Usiombe mwajiri wako akulipe overtime allowance, mwombe akupe muda wa kufanya kazi zako za ziada(perform your own overtime duties)

4. Epuka kuwasambazia pesa za mshahara wako watu wa ukoo wako ili uwaokoe na hali ngumu ya ukosefu wa fedha waliyonayo. Badala yake Wasaidie kuona fursa za kuwapatia Pesa!

5. Usiombe mwajiri wako akuongezee mshahara bali omba Mungu akuwezeshe Kupata kipato endelevu nje ya mshahara wako.

6. Mtu anayeishi kwa kutegemea mshahara wake tu ni sawa na mtu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga na mafuriko yalipokuja anguko la nyumba hiyo lilikuwa na mshindo mkubwa sana.

7. Mto Kagera au Maragalasi haijawahi kukauka maji yake. Kwa nini? Ni kwa sababu inapokea maji yake kutoka kwenye vyanzo vingi vya maji au vijito vingi! Mtu mwenye vyanzo vingi vya mapato zaidi ya mshahara atafanishwa na mto Kagera au Maragalasi isiyokauka maji yake.

8. Usisubiri kustaafu kazi ndipo ulipwe mamilioni ya pesa za kiinua mgongo bali tafuta kumiliki vyanzo sahihi vya pesa, na ndipo malipo ya kiinua mgongo utalipwa kila wiki mamilioni ya pesa.

9. Watu wenye busara hutafuta vyanzo vya pesa vinavyoweza kuwalipa mshahara au pensheni ya Tshs 150 milioni kwa mwezi badala ya kusubiri kulipwa kiinua mgongo cha Shs 150milioni baada ya kufanya kazi kwa miaka 30 au zaidi.

10. Waajiriwa wenye hekima na busara hutumia mishahara yao kutengeneza au kutandaza mabomba ya fedha au mtandao wa fedha endelevu ili hata kama hawatakuwepo tena duniani watoto wao na watoto wa watoto wao waendelee kupata mshahara kila mwezi!

JIFUNZE MAFANIKIO

Jifunze kila siku. Maji yaliyojaa kwenye ndoo hayawezi kukuaa kwenye kikombe yote. Uwezo wako wa sasa na ndoto zako na mafanikio unayoyataka ni tofauti.

Kwa kujifunza kila siku kunakuwezesha wewe ukuze uwezo wako wa kubeba vitu vikubwa.

Nadhani mlishasikia watu wanasema pesa za viwanja hazikai. Pesa za madini zina mashetani
Ukweli ni kwamba hakuna cha mashetani  uwezo wako wa kubeba pesa ni mdogo huna nidhamu ya matumizi ya fedha. Hivyo utabakia vile vile hata ukipewa milioni mia leo zitabakia zile unazoweza kubeba.

Maji yaliyojaa ndoo yakiwekwa yote kwenye kikombe yatamwagika  

Read more   http://ow.ly/H6Wj302uAG6

USIJIONEE HURUMA KUPITILIZA

*HUWEZI KUFANIKIWA KIBIASHARA KAMA UNAPENDA KUJIHURUMIA HURUMIA!*

��Mama mmoja Mzungu alitembelea mlima Kilimanjaro miaka iliyopita. Alikuwa amepanga kupanda mlima Kilimanjaro mpaka kileleni, yaani Kibo na Mawenzi, ili hatimaye apewe cheti cha kupanda mlima mrefu Afrika.

��Lakini kwa bahati mbaya akiwa amefika katikati ya mlima alizidiwa kiafya na hatimaye akashushwa mlimani akiwa amezirai hadi hospitalini.

��Siku ya tatu alipozinduka hospitalini huku marafiki zake wakimpa pole, aliwajibu kuwa “Mlima Kilimanjaro hauwezi kuongezeka urefu, lakini mimi mwanadamu nina uwezo wa kuongeza maarifa, nguvu na mbinu za kupanda milima wowote duniani. Kwa hiyo nitarudi tena wakati mwingine mpaka nipande mlima Kilimanjaro hadi kileleni, ingawa nimepata changamoto wakati huu.”.

��Alivyorudi kwao Marekani, alianza kufanya mazoezi tena ya kukimbia na kupanda vichuguu na vilima kwa muda wa mwaka mzima, na kisha mwaka uliofuata alirudi tena Tanzania, akapanda mlima Kilimanjaro mpaka kilele cha Kibo na mawenzi, na hatimaye akapewa cheti cha kupanda mlima Kilimanjaro!.

��Je huyo mzungu angeamua kusubiri mlima Kilimanjaro upungue urefu ndipo aje Tanzania kuupanda, jambo hilo lingewezekana?

��Je unataka maisha yawe rahisi ndipo uyamudu? Je unataka viwanja vishuke bei ndiyo ujenge nyumba yako? Je unataka ada za shule ziwe chini ndipo usome? Je unataka gharama za hospitali ziwe chini ndipo utibiwe? Je unataka mahari iwe chini ndipo uoe? Je unataka vitabu vya mafunzo ya biashara viwe bei chee ndiyo ununue? Unataka mshahara wako uwe mkubwa ndipo ufanikiwe? Je unataka shetani auwawe ndiyo umche Mungu? Je unataka dunia irudi nyuma, ndipo uweze kuyamudu maisha? Je, unataka urudi tumboni mwa mama yako ili uwe unakula na kulala bure? Ebo!��

��Kama nia yako ni kufanikiwa hutakiwi kujionea huruma, nenda kwa wakati na ujitoe hadi kieleweke.

*Kila la kheri na pia nakutakia MAFANIKIO makubwa sana wewe na kizazi chako, barikiwa sana*

EPUKA VISABABU

�� Unaweza ukajitetea sana jinsi ambavyo hali ni ngumu.

��Unaweza ukajitetea sana jinsi ambavyo huwezi kufikia malengo na ndoto zako lakini ukweli unabaki kwamba hizo sababu na kujitetea hakukubadilishii hali uliyonayo.

�� Uchumi umekua mgumu sana unaweza kutumia hiyo kama sababu ya kujitetea au kama fursa ya kutafuta suluhisho.

☹ Hata Mungu hataki watu wanaojitetea na kutoa sababu kwanini hawawezi na kwanini wamekosea. Kaa kwenye nafasi yako utatue matatizo yako.

��Ifanye akili yako ifikiri. Akili ikishindwa kutumika vyema itatumika vibaya.��

CHUKUA HATUA

��Morning Rise Up��

✍��SABABU KUMI ZINAZO KUFANYA USISONGE MBELE

Wakati tukikuta mambo yetu hayaendi huwa tunadhani kuna mchawi anaiingilia mambo yetu kumbe mchawi wa mambo yetu ni sisi wenyewe  na si vinginevyo .

Zifuatazo ni sababu kumi zinazokufanya usisonge mbele :

1.Huna ndoto : Kama hujui unataka nini katika maisha yako wewe utakuwa ni mtu wa kusubiri Jua lichomoze na kuchwa .Hutakuwa na msukumo wa ndani wa kuhakikisha kuwa siku moja ndoto yako inakuwa kweli .Umekuwa ukifanya vitu kwa mazoea kwa sababu huna ndoto yoyote inayokufanya kuwaza kila siku namna gani utaifikia.

2.Unawasikiliza watu sana kuliko kujisikiliza mwenyewe:Maisha yako ni yako na si ya kaka yako wala mjomba wako au ndugu yeyote na rafiki yeyote uliye naye . Kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe(Every body will carry his own burden).Kama unaamini katika unachokifanya na unajua kitakufikisha mahali endelea kufanya kadri unavyoweza .Watu wengi si wazuri na hawajui unakokwenda japo wanaweza kujua ulikotoa .

3.Hutafuti Maarifa : Bila maarifa hutaenda kokote na maisha yako hayatabadilika .Utakuwa kama mtu anayepiga ngumi ukutani ambapo mwisho wa siku huumiza mkono wake mwenyewe .Kama siyo msomaji wa vitabu ,kuperuzi kwenye mtandao kutembelea blog kama www.kijanajithamini1.blogspot.com na www.maishanamafanikio.blospot.com hautaweza kupata maarifa ambayo yatakufanya ufanye mambo yako kwa uwaredi mkubwa na kwa tofauti .Utakuwa ni mtu wa kufanya mambo kimazoea maana huna maarifa na mwisho wa siku hutatoka pale ulipo.

4.Unajihurumia sana : Umekuwa mtu wa kujihurumia sana na kutaka kukaa kwenye comfort zone ,sehemu ambayo unapata vitu kwa urahisi .Hutaki  kuumiza kichwa na kuwaza juu ya maisha yako .Umekuwa mtu wa kutaka vitu ambavyo vimeshafanywa na wenzio maana hutaki kuteseka  na kukutana na changamoto .

5.Unaishi kwa yaliyopita : Maisha siyo jana maisha ni kesho .Kama ukiangalia ulivyoshindwa jana hutafikiria kuhusu kesho .Ukiangalia biashara ya jana ilivyodhurumiwa na kuibiwa hutafanya biashara kesho .Acha kabisa kuishi kwa ya jana hutasonga mbele .Angalia sana kesho yako , Maisha ya watoto wako wa kesho ,mahusiano na familia yako ya kesho na si vinginevyo .

6.Huchukui hatua : Umekuwa mtu wa kusema nitafanya kesho na kesho ikifiika hufanyi .Umekuwa na mipango mingi isiyokuwa na utekelezaji .Kama huchukui hatua utabaki hapo hapo ulipo  hakuna jambo jipya litakalotokea .

7. Unasubiri Matokeo ambayo hujafanyia kazi ; Usitegemee muujiza .Kile apandacho mtu ndicho atakachovuna .Unawezaje kuvuna mahali ambapo hujapanda??? Hey ! Unawezaje kuvuna maharage kwenye shamba la mahindi???? .Newton anasema ili kazi ifanyike lazima kani (force) itumike na umbali(distance ) uwepo .Hakuna matokeo yasiyosababishwa.

8.Huzalishi mawazo : Umekuwa mtu ambaye hutaki kuwaza kwa mtazamo mpya na kuzalisha mawazo mengi kadri iwezekanavyo .Umeishi kwa wazo la mwaka 1999 mpaka leo na hujui kama dunia imebadilika .Hey! Amka anza kuzalisha mawazo .

9.Umeishi kwa tahadhari nyingi :Kila kitu kwako umechukua tahadhari ,unahisi ukianza biashara fedha zako zitapotea ,unahisi ukianzisha kitu hakitasonga mbele .Kwanini umekuwa hivo (too cautious) ????.Kama hutaachana na tabia hii hutatoka mahali ulipo na kamwe usitafute mchawi .

10.Hujifanyii tathimini :Huna tabia ya kupima yale uliyoyafanya kwa siku,wiki,mwezi na mwaka na hivyo unahisi kama unaenda mbele kumbe unarudi nyuma .Ni muhimu ukawa na tathimini ya mambo yako binafsi.

JITATHMINI...

AMUA LEO

��Morning Rise Up��

✍��"Fimbo iliyo mkononi Ndiyo iuayo nyoka ��".

��Wakati nasoma methali hii sikuwa naielewa hasa nikijiuliza kuwa kama nyoka atakuwa mkubwa Mfano wa chatu�� na mimi nikiwa na fimbo Ndogo Je nitaweza kumuua nyoka??.

��Ilikuwa ngumu sana kuielewa methali hii na nilimsumbua sana mwalimu wangu ili nielewe vizuri. Asante sana kwa Mwalimu kunivumilia kwa maswali ambayo yalilenga mimi kuelewa zaidi.

��Mwalimu alinieleza kuwa "Joas Hata kama utakutana na chatu,silaha ya kwanza utakayo tumia ni ile itakayo kuwa mkononi mwako huku ukitafuta silaha kubwa."  aliendelea kusema "Hata kiatu ulichovaa chaweza kumuua nyoka ".

��Ukweli ni kwamba tumewaza kufanya makubwa ,lakini tumeshindwa kwa sababu Hatuwezi kuvitumia vile vidogo tulivyonavyo kwanza kwa muda huo huku tukisubiri vikubwa.

��Kuna mtu ana kipaji ambacho hata hakihitaji mtaji, lakini mtu huyu kakaa tu akisubiri fedha za muujiza maisha yaanze Kubadilika. Je, Unachukua hatua gani kuonesha jamii kama una kipaji ili jamii ikukubali au umekaa tu ukisubiri mtu aje akutoe Mahali ulipo⁉ Nasikitika kwamba haitawezekana mpaka hapo Wewe  utakapochukua hatua stahiki ya kufanya chochote Unachoweza  kufanya

Hivi unajua Masanja Mkandamizaji alikotoka?Je,asingetumia kipaji chake nani angemuona?? .Hivi Unamjua Mbwana Sammatta⁉ Leo Mbwana Sammatta analipwa mshahara kwa mwezi zaidi ya pension(mafao) yako utakayolipwa baada ya kustaafu kwa kuwa alitumia kipaji alichokuwa nacho. ��

Unaweza Nini⁉ Unapenda kufanya nini⁉Hujui kuna watu ni matajiri kwa uchoraji⁉ Hujui kuna watu ni matajiri kwa kukimbia (riadha),hujui kuimba ni utajiri⁉ .Shida umedharau uwezo wako ambao unaweza kukutajirisha.

Unasubiri nini⁉ Unasubiri mtaji mkubwa⁉ Unasubiri msaada toka nje⁉ .Anza na kinachowezekana huku ukisubiri hayo makubwa unayofikiri.

��Hakuna nyumba ambayo haikuanza na msingi ikiwepo itakuwa ya mchawi.Hivi Kuna Chuo kikuu Bila shule Ya msingi⁉��  .hivi Kuna magunia ya Karanga ambayo hayakutokana na uaminifu wa mkulima kupanda Kile alichokuwa nacho⁉.

SUCCESS

Tips For success.
1.Think Big
From Michelangelo Buonarroti, Great Renaissance Artist: “The greater danger for most of us lies not in setting our aim too high and falling short; but in setting our aim too low, and achieving our mark.”
2.Find what you love to do and do it.
From Oprah Winfrey, Media Mogul: “You know you are on the road to success if you would do your job and not be paid for it.”
3. Learn how to balance life.
From Phil Knight, CEO of Nike Inc.: “There is an immutable conflict at work in life and in business, a constant battle between peace and chaos. Neither can be mastered, but both can be influenced. How you go about that is the key to success.”
4. Do not be afraid of failure.
From Henry Ford, Founder of Ford Motors: “Failure is simply the opportunity to begin again, this time more intelligently.”
5. Have an unwavering resolution to succeed.
From Colonel Sanders, Founder of KFC: “I made a resolve then that I was going to amount to something if I could. And no hours, nor amount of labor, nor amount of money would deter me from giving the best that there was in me. And I have done that ever since, and I win by it. I know.”
6. Be a man of action.
From Leonardo da Vinci, Renaissance Genius : “It had long since come to my attention that people of accomplishment rarely sat back and let things happen to them. They went out and happened to things.”
7. Avoid conflicts.
From Theodore Roosevelt, 26th President of America: “The most important single ingredient in the formula of success is knowing how to get along with people.”
8. Don’t be afraid of introducing new ideas.
From Mark Twain, Famed Author: “A person with a new idea is a crank until the idea succeeds.”
9. Believe in your capacity to succeed.
From Walter Disney, Founder of Walt Disney Company: “If you can dream it, you can do it.”
10. Always maintain a positive mental attitude.
From Thomas Jefferson, 3rd President of America: “Nothing can stop the man with the right mental attitude from achieving his goal; nothing on earth can help the man with the wrong mental attitude.”
11. Don’t let discouragement stop you from pressing on.
From Abraham Lincoln, 16th President of America: “Let no feeling of discouragement prey upon you, and in the end you are sure to succeed.”
12. Be willing to work hard.
From JC Penny, Founder of JC Penney Inc.: “Unless you are willing to drench yourself in your work beyond the capacity of the average man, you are just not cut out for positions at the top.”
13. Be brave enough to follow your intuition.
From Steve Jobs, Co-founder of Apple Inc.: “Have the courage to follow your heart and intuition. They somehow already know what you truly want to become. Everything else is secondary.”